Thursday, March 1, 2018

WAZIRI MKUU AWEKA JIWE LA MSINGI ZAHANATI MBECHA

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiweka jiwe la msingi la Zahanati, iliyopo  katika kijiji cha Mbecha Wilayani Ruangwa, iliyojengwa kwa ufadhili wa Taasisi ya African Relief Organization, wa kwanza kushoto ni Sheikh Abdallah Ndauga (wapili kushoto) ni Mkurugenzi Msaidizi wa Taasisi ya African Relief Organization Sheikh Ibrahim Yusuf, na kulia ni mke wa Waziri Mkuu Mary Majaliwa, Machi 1, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiagana na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Gelasius Gasper Byakanwa, katika kijiji cha Mchenganyumba Wilayani Ruangwa, Waziri Mkuu amemaliza ziara yake ya kikazi Mkoani Mtwara Februari 28, 2018,

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa na Mkewe Mary Majaliwa, wakiwasalimia watoto wa shule ya msingi Mbecha, katika kijiji cha Mbecha Wilayani Ruangwa, Waziri Mkuu yupo Wilayani humo kwa ziara ya kikazi jimboni, Machi 1, 2018.


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkurugenzi Msaidizi wa Taasisi ya African Relief Organization Sheikh Ibrahim Yusuf, iliyojenga Zahanatiiliyopo  katika kijiji cha Mbecha Wilayani Ruangwa, Machi 1, 2018.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimsalimia mtoto Shafii Khamis, katika kijiji cha Mtakuja, Kata ya Nanganga Wilayani Ruangwa, Machi 1, 2018.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akuzungumza na wananchi wa kijiji cha Mtakuja, Kata ya Nanganga Wilayani Ruangwa, Waziri Mkuu yupo Wilayani Ruangwa kwa ziara ya kikazi jimboni, Machi 1, 2018.


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.