Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Bunge na Uratibu) Dkt. Jim Yonazi (mwenyekiti wa kikao) cha Kamati ya Taifa ya Ushauri ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 kilichofanyika tarehe 17 Juni, 2025 katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere JIjini Dar es Salaam.
Kikao hicho kimeudhuriwa na Matibu Wakuu wa
Wizara za Kisekta, Makamisaa wa Sensa pamoja na baadhi ya wakuu wa
Taasisi.Lengo la kikao hicho ni kupokea na kujadili ripoti mbalimbali za
utekelezaji wa Awamu ya Tatu na ya Mwisho ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka
2022.
Aidha miongoni mwa ripoti hizo ni pamoja na
ile ya Utekelezaji wa Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya
Watu na Makazi ya Mwaka 2022 kwa kipindi cha kuanzia Desemba 2024 hadi Mei
2025, na Hali ya Utekelezaji wa Anwani za Makazi.
Pia kikao kimejadili na kupokea Rasimu za
Ripoti Tano za kina za Matokeo ya Sensa, na Ripoti ya Makadirio ya Idadi ya
Watu kuanzia mwaka 2023 hadi 2050 ngazi ya Mikoa.
EmoticonEmoticon
Note: Only a member of this blog may post a comment.