Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya
Uratibu wa Shughuli za Serikali kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu – Sera, Bunge na
Uratibu, Bw. Omary Ilyas, ameongoza kikao maalum cha Wakurugenzi wa Wizara na
Taasisi zinazotekeleza Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo awamu ya pili
(ASDP II).
Kikao hicho kilichofanyika
jijini Dodoma kimejadili utekelezaji wa programu hiyo kwa kipindi cha Julai
2024 hadi Machi 2025, sambamba na kuanza maandalizi ya mpango wa mwaka ujao wa
2025/2026.
Bw. Ilyas amesema ASDP II inalenga kuimarisha usalama wa
chakula, kuongeza tija kwa wakulima na kusaidia ukuaji wa uchumi wa vijijini kupitia
ushirikiano wa kisekta.
Kikao kimehusisha wadau kutoka
sekta ya kilimo, mifugo, uvuvi, pamoja na taasisi za fedha na maendeleo, ili
kuhakikisha utekelezaji wa pamoja unaolenga mafanikio ya mkakati wa Taifa wa
kilimo.
EmoticonEmoticon
Note: Only a member of this blog may post a comment.