Wednesday, June 18, 2025

SERIKALI YAWEKA MIKAKATI YA KUIMARISHA SEKTA YA KILIMO KUPITIA ASDP II

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu wa Shughuli za Serikali kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu – Sera, Bunge na Uratibu, Bw. Omary Ilyas, ameongoza kikao maalum cha Wakurugenzi wa Wizara na Taasisi zinazotekeleza Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo awamu ya pili (ASDP II).

Kikao hicho kilichofanyika jijini Dodoma kimejadili utekelezaji wa programu hiyo kwa kipindi cha Julai 2024 hadi Machi 2025, sambamba na kuanza maandalizi ya mpango wa mwaka ujao wa 2025/2026.

Bw. Ilyas amesema ASDP II inalenga kuimarisha usalama wa chakula, kuongeza tija kwa wakulima na kusaidia ukuaji wa uchumi wa vijijini kupitia ushirikiano wa kisekta.

Kikao kimehusisha wadau kutoka sekta ya kilimo, mifugo, uvuvi, pamoja na taasisi za fedha na maendeleo, ili kuhakikisha utekelezaji wa pamoja unaolenga mafanikio ya mkakati wa Taifa wa kilimo.


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.