Thursday, March 19, 2026

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA AFYA NA MASUALA YA UKIMWI YAIPONGEZA SERIKALI KUWAWEZESHA KIUCHUMI WAISHIO NA VVU

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI ambaye pia ni Mbunge wa Arumeru Magharibi Mhe. Johannes Lukumay ameipongeza  Serikali kuendelea kusaidia kundi la Watu waishio na Maamubikizi Virusi vya UKIMWI kupitia shughuli mbalimbali za kiuchumi ili kujikwamua kiuchumi.

Mhe. Lukumay ameyasema hayo mara baada ya ziara ya kutembelea Baraza la Watu waishio na maambukizi ya Virusi vya UKIMWI akiwa ameambatana na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI katika (Konga ya Jiji) iliyofanyika   katika Viwanja vya Pugu Mnadani Jijini Dar es Salaam.

Amesema kuwa watu waishio na maambukizi ya Virusi vya UKIMWI ni sawa na watu wengine hivyo yapaswa kuwapa kipaumbele katika fursa mbalimbali za kimaendeleo.Pia Mwenyekiti huyo amelipongeza kundi hilo kwa namna wanavyojituma katika kuhakikisha wanajikwamua kiuchumi na kuondokana na umasikini hivyo  kuziagiza  sekta husika kusaidia katika kuwatafutia masoko kwa ajili ya bidhaa zao.

Kwa upande wake Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Mhe. Ummy Nderiananga amesema kuwa Serikali chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan wataendelea kuunga mkono jitihada zao kwa kuongeza nguvu zaidi kwa Wanakonga ili waweze kujikwamua kiuchumi.

Mhe. Nderiananga amempongeza Mkurugenzi wa Jiji, Mkuu wa Wilaya pamoja na Katibu Tawala wa Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam na timu nzima kwa kuwawezesha Wanakonga katika fursa mbalimbali na kuwataka kuendelea na desturi hiyo ya kuwawezesha kwani mwaka huu wa fedha bado haujamalizika.

Aidha Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam Elihuruma Mabelya amesema kuwa moja ya eneo waliloliwekea nguvu ni Konga hiyo kwa kuunga mkono shughuli zao za kiuchumi ili kuhakikisha wanainuka na kufanikiwa katika nyanja mbalimbali za maendeleo




EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.