Friday, December 22, 2017

WAZIRI MKUU AKAGUA KIWANDA CHA JOC SHINYANGA

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa (katikati) akitaka ufafanuzi kuhusu aina ya nyuzi zinazozalishwa na kiwanda cha JOC kutoka kwa Meneja Mkuu wa kiwanda hicho, Bw. Jim Liu katika ziara fupi aliyofanya kiwandani hapo leo asubuhi, Desemba 22, 2017. Wa kwanza kulia ni Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Bibi Maimuna Tarishi na wa pili kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Bi. Zainab Tellack.

 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa (katikati) akipatiwa maelezo na Meneja Mkuu wa kiwanda cha kutengeneza nyuzi cha JOC, Bw. Jim Liu wakati alipozuru kiwanda hicho kuona uzalishaji mjini Shinyanga leo asubuhi, Desemba 22, 2017. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Bi. Zainab Tellack.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiangalia bandali la nyuzi zilizosokotwa na kiwanda cha kutengeneza nyuzi cha JOC, mjini Shinyanga leo Desemba 22, 2017 na kubainishwa kwamba zimetoka Tanzania. Kushoto ni Meneja Mkuu wa Kiwanda hicho, Bw. Jim Liu.


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.