Tuesday, January 28, 2020

BUNGENI LEO TAREHE 28.01.2020

Wanakwaya wa Bunge  wakiimba Wimbo wa Taifa wakati Spika wa bunge, Job Ndugai  alipoafungua Mkutano wa Kumi na Nane wa Bunge jijini Dodoma, Januari 28, 2019.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama, Bungeni jijini Dodoma, Januari 28, 2019.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani, Bungeni jijini Dodoma, Januari 28, 2019.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Mbunge wa Kuteuliwa, Janet Masaburi, Bungeni jijini Dodoma, Januari 28, 2019.
Spika wa Bunge, Job Ndugai  (wa pili kulia) akimvalisha Joho, Spika  wa bunge Mstaafu, Pius Msekwa katika hafla ya kukabidhi majoho kwa Maspika Wastaafu iliyofanyika Bungeni jijini Dodoma, Januari 28, 2019. Kulia ni Katibu wa Bunge, Stephen Kagaigai.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Spika wa bunge Job Ndugai  (aliyekaa wa pili kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na Maspika na Mawaziri Wakuu wastaafu katika hafla ya kukabidhi majoho kwa Maspika wastaafu iliyofanyika Bungeni jijini Dodoma, Januari 18, 2019.  Waliokaa kutoka kushoto ni Mbunge wa Urambo, Magaret Sitta ambaye pia ni Mke wa Spika Mstaafu, Marehemu Samuel Sitta, Spika wa Bunge Mstaafu, Pius Msekwa na kulia ni Spika wa Bunge Mstaafu, Anne Makinda. Waliosimama ni Maziri Wakuu Wataafu, kutoka kushoto ni Frederick Sumaye, Edward Lowassa na John Malecela.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana  na wananchi kutoka Urambo walioambatana na mbunge wao, Margaret Sitta katika hafla ya kukabidhi majoho kwa Maspika wastaafu iliyofanyika Bugeni jijini Dodoma, Januari 28, 2019.



EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.