Tuesday, January 2, 2018

KATIBU MKUU OFISI YA WAZIRI MKUU ATEMBELEA NYUMBA ZA TBA DODOMA

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Prof. Faustin Kamuzora (kushoto) akimsikiliza Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu wa Shughuli za Serikali Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Obey Assery wakati alipotembelea Mradi wa Nyumba za Kikuyu Flats zinazosimamiwa na  Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Dodoma Januari 2, 2018.

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Prof. Faustin Kamuzora (kushoto) pamoja na Mkurugenzi wa Uratibu wa Shughuli za Serikali Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Obey Assery wakiangalia baadhi ya majengo yanayokarabatiwa kwa ajili ya Watumishi wa Serikali watakao hamia Dodoma  alipotembelea Kukagua ukarabati huo Januari 02, 2018.

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Prof. Faustin Kamuzora akitoa maelekezo kwa Mkurugenzi wa Idara ya  Uratibu wa Shughuli za Serikali wa Ofisi hiyo Bw. Obey Assery kuhusu ukarabati wa nyumba za Kikuyu Dodoma alipotembelea kuangalia ukarabati wa nyumba hizo Januari 02, 2018.

Muonekano wa moja ya jengo lililokarabatiwa chini ya Usimamizi wa Wakala wa Majengo (TBA) lililopo eneo la Kikuyu Flats Dodoma


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.