Saturday, January 20, 2018

WAZIRI MKUU ATEMBELEA SHAMBA LA JKT RWAMKOMA

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amekagua shamba la uzalishaji wa mbegu bora za mihogo aina ya mkombozi linalomilikiwa na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kikosi cha Rwamkoma wilayani Butiama.

Amekagua shamba hilo linalomilikiwa na Kikosi cha JKT Rwamkoma leo (Jumamosi, Januari 20, 2018) alipowasili wilayani Butiama akiwa katika ziara ya kikazi mkoani Mara. Kikosi hicho kimewezeshwa na Halmashauri ya Butihama.
Waziri Mkuu amewakipongeza kikosi cha JKT Rwamkoma kwa uamuzi huo wa kuzalisha mbegu bora za mihogo ambazo baadae zitasambazwa kwa wakulima wa zao hilo wilayani hapa.
Pia amewataka wakazi wanaoishi karibu na shamba la kikosi hicho hilo kulitumia kama shamba darasa kwa ajili ya kujifunza namna bora ya kulima zao hilo.
Kwa upande wake Mkuu wa Kikosi hicho Luteni Kanali David Msakulo alisema shamba hilo linaukubwa wa ekari 60, na mbegu zitakazozalishwa zitatosha kupanda ekari 900.
Mkuu huyo wa kikosi hicho aliongeza kuwa mbegu hizo zinazozalishwa katika shamba hilo zitagawanywa kwa wakulima katika kata zote 18 za wilaya ya Butihama.
Alisema mbali ya kuzalisha mbegu pia wanatarajia kuanzisha kiwanda cha kuchakata zao la mihogo ili kuweza kuliongezea thamani.
Mbali na shamba la mbegu bora za mihogo pia kikosi hicho  kina shamba lingine la pamba lenye ukubwa wa ekari 57, ambapo wanatarajia kuvuna tani 57 za pamba. Mwakani wanatarajia kuongeza ukubwa wa shamba na kufikia ekari 300.
Awali,  Waziri Mkuu alitembelea shamba darasa la mkoa wa Mara la zao la pamba lililopo Kisangwa wilayani Bunda akiwa njiani kuelekea wilayani Butihama, kuendelea na ziara yake ya kikazi mkoani Mara.
Mkuu wa Mkoa wa Mara, Bw. Adam Malima alisema shamba darasa hilo ni moja ya jitihada za Mkoa wa Mara kuelimisha wakulima wa zao hilo mbinu bora za uzalishaji ili kuongeza tija katika uzalishaji.


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.