Sunday, September 23, 2018

MAJALIWA ASHIRIKI MAZISHI YA WALIOFARIKI DUNIA KATIKA AJALI YA KIVUKO CHA MV NYERERE

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimia na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama  wakati alipowasili katika kijiji cha Bwasa kwenye  kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe kushiriki katika mazishi ya wananchi waliofariki dunia katika ajali ya kivuko cha MV Nyerere, Septemba 23, 2018.

 Askari wakiweka kaburibi miili ya baadhi ya  wananchi walifariki dunia katika ajali ya Kivuko cha MV Nyerere kilichozama kwenye  kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe wakati wa   mazishi yaliyoongozwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa katika kijiji cha Bwisa kisiwani Bukara, Septemba 23, 2018.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Naibu Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi na Mbunge wa Ilemela, Angelina Mabula na viongozi wengine walioshiriki katika mazishi ya  baadhi ya wananchi waliofariki dunia katika ajali ya meli ya MV Nyerere katika kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe Septemba 23, 2018.

Wahandisi na mafundi wakifanya juhudi kubwa za kukivuta kivuko cha MV Nyerere ambacho kilizama katika kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe .Baadhi Wananchi waliofariki dunia katika ajali hiyo walizikwa katika mazishi yaliyoongozwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kwenye kijiji cha Bwasa kisiwani Ukara Septemba 23, 2018.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mohammed Abood  (wapili kulia) akiungana na Masheikh katika  sala kwenye mazishi ya wananchi waliofariki dunia katika ajali ya Kivuko cha MV Nyerere kilichozama katika Kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe. Mazishi hayo yaliongozwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa katika kijiji cha Bwisa  kisiwani Bukara, Septemba 23, 2018.


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.