Monday, September 3, 2018

MAJALIWA AKUTANA NA WAZIRI WA KILIMO WA CHINA

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Waziri wa Kilimo wa China, Bw.  Han Changfu (kushoto) wakati alipotembelea Wizara hiyo iliyopo Beijing, Septemba 3, 2018.

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Waziri wa Kilimo wa China, Bw. Han Chanfu  wakishuhudia utiaji saini wa Makubaliano ya Ushirikiano katika masuala ya Uvuvi kati ya China na Tanzania kwenye ukumbi wa Wizara ya Kilimo ya China katika jiji la  Beijing, Septemba 3, 2018. Wanaotia Saini ni Waziri wa Kilimo, Mifugo na  Uvuvi wa Zanzibar, Rashid Ali Juma (kushoto) na Naibu Waziri wa Kilimo wa China, Qu Dongyu.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Waziri wa Kilimo wa China, Bw. Han Changfu wakati alipotembelea Wizara ya Kilimo ya nchi hiyo iliyopo Beijing Septemba 3, 2018.  Majaliwa yupo nchini China kumwakilisha Rais John Pombe Magufuli katika Mkutano wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya Afrika na China - FOCAC.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Kilimo wa China, Bw. Han Chanfu (wanne kulia)  na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki, Dkt. Augustine Mahiga (kushoto) baada ya mazungumzo yao kwenye ukumbi wa wizara hiyo jijini Beijing, Septemba 3, 2018. Wengine pichani ni  Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi  wa Zanzibar,  Rashid Ali Juma. (wapili kushoto), Balozi wa China nchini Tanzania, Wang Ke (watatu kushoto), Balozi wa Tanzania nchini China, Mbelwa Kairuki na Naiba Waziri wa Kilimo wa China, Qu Dongyu.

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na ujumbe wake wakiagana na viongozi wa Wizara ya Kilimo ya China baada ya mazungumzo yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Wizara hiyo, Beijing nchini China, Septemba 3, 2018.


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.