Tuesday, February 4, 2020

WAZIRI MHAGAMA AWAFUNDA WATUMISHI WA OFISI YA WAZIRI MKUU

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akizungumza wakati wa ufunguzi wa  kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa ofisi yake kilichofanyika Februari 3, 2020 Jijini Dodoma , kushoto kwake ni Mwenyekiti wa baraza hili Bw. Tixon Nzunda ambaye ni Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo anayeshughulikia masuala ya Waziri Mkuu na Bunge , na kulia ni katibu wa baraza hilo Bw. Paschal Vyagusa.

Katibu wa Baraza la Wafanyakazi la Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Paschal Vyagusa akieleza jambo wakati wa kikao hicho.
Mjumbe wa Baraza la Wafanyakazi la Ofisi ya Waziri Mkuu Bi. Ernajoyce Hallo akichangia jambo kuhusu umuhimu wa chanjo ya homa ya ini (hepatitis B) kwa watumishi ili kuwa na afya njema wakati wa kikao hicho.
Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Ununuzi na Ugavi Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Joachim Zaharani akiwasilisha mada ya Mfumo wa kielekitroniki wa ununuzi wakati wa kikao cha baraza la wafanyakazi la ofisi hiyo lililofanyika tarehe 3 Februari, 2020 Dodoma.
Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi la Ofisi ya Waziri Mkuu ambaye ni Katibu Mkuu Bw. Tixon Nzunda akizungumza wakati wa kikao hicho Jijini Dodoma.
Wajumbe wa Sekretarieti ya kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa ofisi ya Waziri Mkuu  wakinukuu hoja wakati wa kikao hicho.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akizungumza na wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wakati wa kikao chao cha kwanza cha mwaka kilichofanyika Februari 3, 2020 Jijini Dodoma.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akizungumza wakati wa ufunguzi wa  kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa ofisi yake kilichofanyika Februari 3, 2020 Jijini Dodoma , kushoto kwake ni Mwenyekiti wa baraza hili Bw. Tixon Nzunda ambaye ni Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo anayeshughulikia masuala ya Waziri Mkuu na Bunge , na kulia ni katibu wa baraza hilo Bw. Paschal Vyagusa.
Sehemu ya wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakifuatilia hoja za kikao kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi hiyo jijini Doodma.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama pamoja na Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi la ofisi hiyo Bw. Tixon Nzunda kushoto kwake waliokaa, na Katibu wa TUGHE Mkoa wa Dodoma Bw. Anthelmu Tarimo (kulia kwa waziri) pamoja na katibu wa baraza hilo Bw. Paschal Vyagusa wa kwanza kushoto waliokaa, wakiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa baraza mara baada ya kikao hicho kufunguliwa rasmi Jijini Dodoma.




EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.