Monday, April 30, 2018

KATIBU MKUU OFISI YA WAZIRI MKUU ATEMBELEA BOHARI KUU YA DAWA MSD

Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa Rugambwa Bwanakunu akitoa maelezo kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Prof. Faustin Kamuzora baada ya kuingia kwenye mojawapo ya Ghala la kuhifadhia madawa katika ofisi za Bohari ya Dawa Jijini Dar es salaam tarehe 30 Aprili, 2018. Bwanakunu alimuelezea katibu mkuu kuwa Bohari ya Dawa inahudumia vituo 7309 nchi nzima katika usambazaji wa Dawa.
Mojawapo ya sehemu ya Ghala linalohifadhi Dawa kwa kutumia Mfumo wa kieletroniki katika Bohari kuu ya Dawa (MSD) Jijini Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya ziara ya Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu kutembelea Bohari hiyo na kujionea namna wanavyo fanyakazi.
Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa Rugambwa Bwanakunu akimueleza jambo Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Prof. Faustin Kamuzora baada ya kuwasili na kwenda kutembelea moja ya ghala la kuhifadhia Dawa katika ofisi za Bohari ya Dawa tarehe 30 Aprili, 2018 Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Prof. Faustine Kamuzora akisisitiza jambo wakati akifanya mazungumzo na viongozi wa Bohari ya Dawa alipowatembelea leo katika Ofisi zao Jijini Dar es salaam April 30,2018.  Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa Rugambwa Bwanakunu.



EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.