Tuesday, April 3, 2018

MAJALIWA AZINDUA MBIO ZA MWENGE GEITA

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipunga mkono kwa wananchi wakati aliposhiriki sherehe za kuwasha  Mwenge wa Uhuru,leo katika uwanja wa Magogo ,mjini Geita.
 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Jenista Mhagama akizungumza katika sherehe za kuzindua mbio za Mwenge wa Uhuru kwenye uwanja wa Magogo mjini Geita, Aprili 2,  2018. Mgeni rasmi katika sherehe hizo alikuwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama (wapili kulia) wakimsikiliza  Mkuu wa Mkoa wa Geita, Robert Gabriel  wakati alipotoa  salamu za mkoa huo katika sherehe za kuzindua mbio za Mwenge wa Uhuru kwenye uwanja wa Magogo mjini Geita Aprili 2, 2018.

Watoto wakionyesha halaiki katika sherehe za kuzindua mbio za Mwenge wa Uhuru zilizoongozwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kwenye uwanja wa Magogo mjini Geita, Aprili 2, 2018.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwasha Mwenge wa Uhuru kuzindua mbio zake kwenye uwanja wa Magogo mjini Geita, Aprili 2, 2018 Kushoto ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Jenista Mhagama.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimkabidhi Mwenge wa Uhuru kiongozi wa vijana  sita watakaokimbiza Mwenge huo,Charles Kabeho wakati alipozindua mbio za Mwenge wa Uhuru kwenye uwanja wa Magogo mjini Geita, Aprili 2, 2018. Wapili kulia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Jenista Mhagama. 


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.