Saturday, April 6, 2019

VIJANA WAPONGEZA SERIKALI KUWAJENGEA UWEZO KUHUSU KILIMO CHA KITALU NYUMBA

Moja ya Kitalu Nyumba cha mafano katika Wilaya ya Chamwino kama Kinavyoonekana ikiwa ni moja ya mikakati ya kuwainua vijana kupitia  programu ya uwezeshaji inayotekelezwa na Ofisi ya Waziri Mkuu.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi (Wenye Ulemavu) Mhe. Stella  IKupa akifurahia jambo na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Mhe. Nagma Giga akizungumza wakati wa ziara ya wabunge wa kamati hiyo Wilayani Chamwino Dodoma kujionea utekelezaji wa   Programu ya ujenzi wa vitalu nyumba.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana na Ajira) Mhe. Antony Mavunde akiwa pamoja na Makamu Mwenyekiti   wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Mhe. Nagma Giga wakiwa ndani ya moja ya vitalu nyumba hivyo.
Mtendaji  Mkuu wa Kampuni ya Holly Green Agric Mhandisi Octavian Lasway akitoa maelezo kwa wajumbe wa Kamati  ya kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kuhusu namna walivyoweza kutekeleza Programu ya ujenzi wa vitalu nyumba katika halmashauri ya Wilaya ya Chamwino pamoja na kuwajengea uwezo vijana ili kufanya mpango huo unaotekelezwa na Ofisi ya Waziri mkuu.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana na Ajira) Mhe. Antony Mavunde akisisitiza jambo wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria wakati wa ziara ya kamati hiyo kutembelea mradi wa ujenzi wa vitalu nyumba katika Wilaya ya Chamwino Jijini Dodoma Aprili 06, 2019.
Sehemu ya Vijana zaidi ya 100 wa Wilaya ya Chamwino walionufaika na Programu ya ujenzi wa vitalu nyumba katika kila halmashauri hapa nchini wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wajumbe wa Kamati hiyo.
Sehemu ya miche ya nyanya katika kitalu nyumba kama inavyoonekana katika picha ikiwa tayari kumika katika kitalu nyumba.
Muonekano  nyanya katika moja ya vitalu nyumba vilivyotembelewa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria katika Wilaya ya Dodoma mjini.
Mkurugenzi wa Ajira kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Vijana Ajira na Wenye Ulemavu  Bw. Ally Msaki akiwa kwenye moja ya kitalu nyumba wakati wa ziara ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria  katika Wilaya ya Dodoma mjini na Chamwino.


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.