Tuesday, June 26, 2018

KIKOSI KAZI CHA MPANGO WA SERIKALI KUHAMIA DODOMA CHATEMBELEA HOSPITALI YA BENJAMIN MKAPA DODOMA

Kaimu Mkurugenzi Huduma za Uuguzi Hospitali ya Benjamin Mkapa Dkt.Salome Kassanga akitoa maelezo kuhusu wodi maalum ya viongozi wa Serikali iliyopo katika hospitali hiyo kwa wajumbe wa Kikosi kazi cha Kuratibu Mpango wa Serikali kuhamia Dodoma walipotembelea Juni 25, 2018.

Baadhi ya wajumbe wa Kikozi kazi cha Kuratibu Mpango wa Serikali kuhamia Dodoma wakipata maelezo ya kuhusu hospitali ya Benjamini Mkapa kutoka kwa Msimamizi Mkuu wa hospitali hiyo Dkt. walipotembelea Juni 25, 2018 Dodoma.

Baadhi ya wananchi wakipata huduma katika dirisha la mapokezi hospitali ya Benjamin Mkapa iliyopo Chuo kikuu cha Dodoma.

Kaimu Mkurugenzi Huduma za Uuguzi Hospitali ya Benjamin Mkapa Dkt. Salome Kassanga akitoa maelezo kwa baadhi ya wajumbe wa Kikozi kazi cha Kuratibu Mpango wa Serikali kuhamia Dodoma walipotembelea hospitali hiyo kuona namna walivyojipanga katika utoaji wa huduma ya afya nchini.

Kaimu Mkurugenzi Huduma za Uuguzi Hospitali ya Benjamin Mkapa Salome Kassanga akitoa maelezo ya matumizi ya mitambo ya kuchunguza, kuzibua na Kutibu mishipa ya moyo  iliyopo katika Hospitali hiyo walipotembelea kuona namna walivyojipanga katika utoaji wa huduma ya afya nchini.

Muonekano wa mashine za upasuaji wa matundu madogo (endoscopys) vilivyofungwa katika Hospitali ya Benjamin Mkapa Dodoma kwa ajili ya kuhudumia wananchi.

Muonekano wa mashine ya CT-Scaniliyofungwa katika katika Hospitali ya Benjamin Mkapa Dodoma.

Muonekano wa Hospitali ya Benjamini Mkapa iliyopo Dodoma.

Katibu wa Kikosi kazi cha kuratibu Mpango wa Serikali kuhamia Dodoma Bw.Meshach Bandawe (katikati) akipata maelezo kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi Huduma za Uuguzi Hospitali ya Benjamin Mkapa Salome Kassanga juu ya matumizi ya mashine za upimaji wa mfumo wa chakula (Fluoroscopy) iliyopo katika hospitali hiyo Juni 25,2018.

Kaimu Mkurugenzi Huduma za Uuguzi Hospitali ya Benjamin Mkapa Salome Kassanga akionesha sehemu ya ujenzi unaoendelea katika hospitaliya Benjamin Mkapa ikiwa ni moja ya Mpango wa kuongeza jengo la kutolea huduma za afya.


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.