Saturday, June 30, 2018

MAJALIWA AFUNGUA JENGO LA BIASHARA LA NHC LA SINGIDANI MJINI SINGIDA

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Viongozi wa Dini wakati alipowasili kwenye viwanja vya Jengo la Biashara la Singidani lililojengwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) mjini Singida, kufungua jengo hilo Juni 30, 2018. Kulia ni Kaimu Sheikh wa Mkoa wa Singida,  Issa Ramadhani Simba na watatu kulia ni Askofu Edward Mapunda wa Jimbo Katoliki la Singida.

Baadhi ya wananchi na wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipozungumza kabla ya kufungua Jengo la Biashara la NHC la Singidani mjini Singida Juni 30, 2018.

Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Felix Manyama Maagi akisoma taarifa ya Shirika hilo mbele ya mgeni rasmi Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa katika tukio la ufunguzi wa Jengo la Biashara la Singidani lililojengwa na NHC mjini Singida Juni 30, 2018.

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Rehema  Nchimbi akitoa salamu za mkoa mbele ya mgeni rasmi Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa katika tukio la  ufunguzi wa Jengo la Biashara la Singidani lililopo Singada mjini Juni 30, 2018.

Kikundi cha Kwaya cha Polisi Jamii cha Mjini Singida kikiimba mbele ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  katika uzinduzi wa Jengo la Biashara la Singidani lililojengwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) mjini Singida Juni 30, 2018.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiteta na Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi wakati alipofungua Jengo la Biashara la Singidani lilijengwa na Shirika la Taifa la Nyumba (NHC) mjini Singida Juni 30, 2018.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza wakati alipofungua Jengo la Biashara la Singidani lililojengwa na Shirika  la Nyumba la Taifa  (NHC) mjini Singida Juni 30, 2018.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akifungua Jengo la Biashara la Singidani lililojengwa na Shirika la  Nyumba la Taifa (NHC) mjini Singida Juni  30, 2018.  Watatu kulia ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi na wapili kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Rehema Nchimbi. Watatu kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Felix Manyama Maagi na kushoto ni Mbunge wa Viti Maalum Neema Mgaya.  Wanne kushoto ni Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Singida Juma Kilimba na wapili kulia ni Mbunge wa Singida Mjini Mussa Sima. (

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wakimsikiliza, Kaimu Mkurugenzi wa Ubunifu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Margaret Ezekiel wakati alipotoa Maelezo kuhusu Jengo la Biashara la Singidani lililojengwa na NHC mjini Singida na kufunguliwa na Waziri Mkuu Juni 30, 2018.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na wabunge walioshiriki katika ufunguzi wa Jengo la Biashara la Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) la SIngidani mjini Singida Juni 30, 2018. Waliokaa, watatu kushoto ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi, Watano kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Rehema Nchimbi, Wasita kushoto ni Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Singida, Juma Kilimba na  kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Felix Manyama Maagi.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiagana na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi baada ya kufungua Jengo la Biashara la Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) mjini Singida, Juni 30, 2018.


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.