Saturday, November 30, 2019

WAZIRI MHAGAMA AKAGUA MAANDALIZI YA SHEREHE ZA UHURU MWANZA.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama pamoja na wajumbe wa kamati ya maandilizi ya Sherehe ya Uhuru zitakazofanyika Kitaifa Mkoa wa Mwanza wakiwasili kwa ajili ya Ukaguzi wa Uwanja wa CCM Kilumba utakaotumika kwa ajili ya sherehe hizo.Alitembelea tarehe 30 Novemba 2019.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akisalimiana na Afisa Maadhimishi kutoka ofisi yake, Bw.Stephen Magoha alipowasili katika Kijiji cha Hunghumalwa Wilayani Kwimba Mkoani Mwanza ili kukagua jeshi la jadi (sungusungu) walioandaliwa kwa ajili ya kufanya onesho lao wakati wa kilele cha sherehe za Uhuru (9 Desemba, 2019)
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akizungumza na wajumbe wa Jeshi la Jadi (Sungusungu) alipowatembelea Novemba 30, 2019 kukagua maandalizi ya onesho maalum linalohusu shughuli za ulinzi na amani wanazofanya ambalo litaoneshwa wakati wa Maadhimisho ya Sherehe za miaka 58 ya Uhuru, Jeshi hilo lipo Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza.
Mkuu wa Itifaki Balozi Kanali Wilbert Ibuge akizungumza na Jeshi la Jadi (hawapo pichani) wanaoendelea na maandalizi ya onesho maalumu katika sherehe za Uhuru mwaka huu mkoani Mwanza.
Mkuu wa Wilaya ya Kwimba Mhe. Senyi Ngaga na Mtemi wa Sungusungu wa Wilaya hiyo Bw. Mogan Shimbi wakimsikiliza Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama wakati wa ziara yake kukagua maandalizi ya onesho maalum la sungusungu katika wilaya hiyo.
Sehemu ya wajumbe walioshiriki kukagua onesho la sungusungu Wilaya ya Kwimba (hawapo pichani) ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Maadhimishi ya miaka 58 ya Uhuru kwa mwaka 2019.
Sehemu ya wajumbe walioshiriki kukagua onesho la sungusungu Wilaya ya Kwimba (hawapo pichani) ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Maadhimishi ya miaka 58 ya Uhuru.
Baadhi ya wajumbe wa Jeshi la Jadi (sungusungu) wakiimba mbele ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama pamoja na viongozi alioambatana nao wakati wa ukaguzi wa maandalizi ya Maadhimishi ya 9 Desemba, 2019 mkoani Mwanza.
Mtemi wa Sungusungu wa Wilaya Kwimba mkoani Mwanza Bw.Mogan Shimbi akiwaongoza wajumbe wa jeshi hilo kuimba wimbo ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya onesho lao la Maadhimisho ya miaka 58 ya Uhuru na miaka 57 ya Jamhuri.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama pamoja na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, Christopher Derek wakiangalia Gwaride la vikosi vya ulinzi na usalama nchini ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Sherehe Uhuru kwa mwaka 2019.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama pamoja na wajumbe wa kamati ya maandilizi ya Sherehe ya Uhuru wa Mkoa wa Mwanza wakiangalia maandalizi ya Gwaride la vikosi vya ulinzi na usalama nchini ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Sherehe hizo.


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.