Wednesday, July 4, 2018

MAJALIWA AFUNGUA MAONYESHO YA 42 YA BIASHARA YA KIMATAIFA YA DAR ES SALAAM

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizindua Kitabu cha Mwongozo wa Taratibu za Kujenga Kiwanda Nchini Tanzania baada ya kufungua Maonyesho ya 42 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es salaam Julai 4, 2018. Watatu Kulia ni Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage na kulia ni Waziri wa TAMISEMI Suleiman Jafo. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda na wapili kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (Tan Trade), Edwin Rutaberuka. 

Waziri  Mkuu, Kassim Majaliwa akikata utepe  ikiwa ni ishra ya kukabidhi matrekta 560 yaliyonunuliwa na wadau mbalimbali wa kilimo nchini katika maonyesho ya 42 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es salaam Julai 4, 2018.  Watatu kulia ni Waziri wa Viwanda, Biashara ya Uwekezaji, Charles Mwijage na kushoto ni Naibu Waziri wake, Mhandishi Stella Manyanya. Wapili kulia ni Waziri wa Kilimo, Dkt. Charles Tizeba na kulia ni Naibu Waziri wake, Dkt, Mary Mwanjelwa.

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage (kulia) wakitazama trekta lenye uwezo wa kupanda mbegu mbalimbali lili tengenezwa na Kampuni ya CRMATEC ya  Arusha baada ya Waziri Mkuu, kufungua Maonyesho ya 42 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es salam. Julai 4, 2018.


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.