Monday, July 30, 2018

WAZIRI MKUU AWASIMAMISHA KAZI WATUMISHI WATATU KASULU

*Ni wale wanaotuhumiwa kwa wizi wa dawa 

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewasimamisha kazi watumishi watatu wa hospitali ya wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma kwa tuhuma za wizi dawa na vifaa tiba.

Pia Waziri Mkuu ameahidi kuyafunga maduka yote ya dawa yanayodaiwa kununua dawa kutoka kwa watumishi wa hospitali hiyo wasioukkuwa waaminifu na kuziuza kwa wananchi.

Waziri Mkuu amewasimamisha kazi watumishi leo (Jumatatu, Juni 30, 2018) wakati alipotembelea hospitali ya wilaya hiyo akiwa katika ziara yake ya kikazi mkoani Kigoma.

Amewataja watumishi wanaotuhumiwa kuhusika na wizi huo kuwa ni Mfamasia wa wilaya Bw. Michael Nindi, mtumishi wa maabara Bw. Tilas Mbombwe na Bibi. Venansia Batega  ambaye ni muuguzi.

“Watumishi hawa nimewasimamisha kazi kuazia leo hii, ili wapisha uchunguzi wa upetevu wa dawa na vifaa tiba zikiwemo darubini mbili. Hospitali hii inamatatizo makubwa sana ya wizi,”.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amewataka watumishi wa umma kutenga siku tatu katika wiki na kuwafuata wananchi waishio vijijini kwa ajili ya kusikiliza kero zao na kuzipatia ufumbuzi.

Pia Waziri Mkuu amewataka watumishi hao waondoe urasimu wanaouweka kwa lengo la kupokea rushwa na pia wawatumikie wananchi bila ya ubaguzi wa aina yoyote. 

“Sitarajii kusikia jambo hilo kwa sababu halina nafasi. Vyombo vinavyosimamia maadili ya utumishi vitimize wajibu wake ili kuwalinda wananchi wasiingizwe katika utoaji rushwa,”.


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.