Saturday, July 7, 2018

MAJALIWA AHUTUBIA MAADHIMISHO YA SIKU YA USHIRIKA DUNIANI- UWANJA WA FURAHISHA MWANZA

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na watumishi wa TANESCO wakati alipotembelea banda lao katika maonyesho ya siku ya Ushirika duniani yaliyofanyika kitaifa kwenye uwanja wa furahisha jijini Mwanza  Julai 7, 2018.  Wapili kushoto ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack na watatu kushoto ni Naibu Waziri wa Kilimo, Dkt. Mary Mwanjelwa.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama kahawa iliyotengwa katika madaraja mbalimbali wakati alipotembelea banda la Chama cha Ushirika cha Mkoa wa Kagera katika Maonyesho ya Siku ya Ushirika duniani yaliyofanyika kitaifa kwenye uwanja wa Furahisha jijini Mwanza Julai 7, 2018.  Kushoto ni Meneja wa Mauzo ya Nje wa Chama hicho, Joseph Katabalo.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama pamba  na mafuta yanayotokana na mbegu za pamba wakati alipotembelea banda la Ushirika wa wilaya ya Chato katika maonyesho ya Ushirika yaliyofanyika kitaifa  kwenye uwanja wa Furahisha jijini Mwanza Julai 7, 2018.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea kutoka kwa Mwenyekiti wa Shirikisho la Ushirika nchini, Bibi Renata Mwageni (kushoto) Tuzo ya  Rais John Pombe Magufuli iliyotolewa na Wanaushirika nchini  ili kutambua mchango wa Rais  katika kuendeleza sekta ya ushirika na kuinua uchumi wa wananchi wa Tanzani ya 2018 . Makabidhiano hayo yalifanyika kwenye  Maadhimisho ya Siku ya Ushirika Duniani yaliyofanyika kitaifa kwenye  uwanja wa Furahisha jijini Mwanza Juni 7, 2018.  Wapili kushotoi ni Waziri wa Kilimo, Dkt. Charles Tizeba na kulia ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza na na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab  Telack.

Msanii wa kikundi cha sanaa cha Buyegi, John Riziki akicheza ngoma ya nyoka katika Maadhimisho ya Siku ya Ushirika Duniani yaliyofanyika kitaifa kwenye uwanja wa Furahisha jijini Mwanza, Julai 7, 2018.  Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo alikuwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

Msanii wa kikundi cha sanaa cha Buyegi, John Riziki akicheza ngoma ya nyoka katika Maadhimisho ya Siku ya Ushirika Duniani yaliyofanyika kitaifa kwenye uwanja wa Furahisha jijini Mwanza, Julai 7, 2018.  Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo alikuwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

Waziri wa Kilimo, Dkt. Charles Tizeba akizungumza wakati alipomkaribisha Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kuhutubia katika Maadhimisho ya siku ya Ushirika duniani yaliyofanyika kitaifa kwenye uwanja wa  Furahisha jijini Mwanza, Julai 7, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim  Majaliwa akizungumza katika Maadhimisho ya siku ya ushirika duniani yaliyofanyika kitaifa  kwenye uwanja wa Furahisha jijini Mwanza, Julai 7, 2018.

Baadhi ya wananchi waliohudhuria katika Maadhimisho ya  Siku ya Ushirika duniani  wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipohutubia kwenye uwanja wa Furahisha jijini Mwanza Julai 7, 2018.


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.