Sunday, January 6, 2019

SERIKALI YAZIPA KANDARASI YA THAMANI YA 2.9BN KAMPUNI ZA VIJANA KUTEKELEZA MAFUNZO YA KILIMO CHA KITALU NYUMBA

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana na Ajira) Mhe.Anthony Mavunde akizungumza na watendaji wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine pamoja na viongozi walioshiriki katika warsha ya uzinduzi wa Mafunzo kwa wakufunzi ya kilimo cha Kitalu Nyumba (Green House) yanayoendelea kwa siku tano katika Chuo hicho mkoani Morogoro.kushoto kwake ni Naibu waziri wa ofisi hiyo, anayeshughulikia wenye ulemavu Mhe.Stella Ikupa
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana na Ajira) Mhe.Anthony Mavunde pamoja na Mhe.Stella Ikupa (Wenye Ulemavu) wakiangalia karatasi inayotumika kama  kifungashio cha unga unaotengenezwa kwa viazi lishe.

Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Royal Agri.Co.ltd Bw. Jonathan Sangau akitoa maelezo kwa Manaibu Waziri kuhusiana na vifaa vinavyotumika katika  kufungia vitalu nyumba

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana na Ajira) Mhe.Anthony Mavunde akimwaga zege kwa ajili ya kutengeneza vitalu nyumba kama ishara ya uzinduzi wa mradi huo.

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana na Ajira) Mhe.Anthony Mavunde akiangalia mapapai yaliyolimwa kwa njia ya kisasa katika mashamba ya SUGECO katika Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine Morogoro.

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana na Ajira) Mhe.Anthony Mavunde akipewa maelezo na Mtaalamu wa masuala ya lishe (SUGECO) Jolenta Joseph kuhusu ukaushwaji wa viazi lishe wakati akikagua kaushio la jua (solar dryer).
Mkurugenzi wa Ajira Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana na Ajira) Bw. Ally Msaki  akizungumza wakati wa uzinduzi huo.


Manaibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu wakiangalia kiazilishe katika moja ya banda la maonesho la vijana walioshiriki mafunzo ya Kilimo cha kisasa cha kitalu nyumba. Katikati ni Mhe.Stella Ikupa anayeshughulikia Wenye Ulemavu na Kushoto ni Mhe.Anthony Mavunde

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana na Ajira) Mhe.Anthony Mavunde akizungumza na mtaalamu wa masuala ya kilimo cha kisasa kwa  kutumia mabwawa ya samaki (Acquculte) alipotembelea kukagua mradi huo, wa kwanza kulia ni Naibu Waziri Ofisi hiyo Mhe Stella Ikupa



EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.