Thursday, January 10, 2019

ZIARA YA WAZIRI MHAGAMA OFISI ZA PSSSF NA NSSF MOSHI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.Jenista Mhagama (kushoto) akimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe.Anna Mghwira wakati wa ziara yake ya kukagua utekelezaji wa maagizo ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Magufuli kwa mifuko ya hifadhi ya jamii NSSF na PSSSF aliyoyatoa Desemba 28, 2018 alipokutana na viongozi wa Shirikisho la vyama vya wafanyakazi Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.Jenista Mhagama (kulia) akimsikiliza Meneja wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa PSSSF Bi. Neema Kuwite wakati wa ziara yake katika ofisi hizo Januari 10, 2019.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.Jenista Mhagama akimsalimia Bi.Mary Kiramvu  mmoja wa wastaafu waliojitokeza kuhakiki taarifa zake katika Ofisi za PSSSF Moshi ikiwa ni utekelezaji wa majukumu ya Mhe.Rais alipokutana na viongozi wa Shirikisho la vyama vya wafanyakazi Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.Jenista Mhagama akifurahi na baadhi ya wastaafu walioripoti katika ofisi za PSSSF Moshi wakati wa zoezi uhakiki wa taarifa za uanachama ili kubaini wastaafu hewa.
Baadhi ya wastaafu wakijaza fomu za taarifa zao wakati wa zoezi la uhakiki katika ofisi za PSSSF Moshi  mkoani Kilimanjaro Januari 10, 2019.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.Jenista Mhagama akizungumza jambo na baadhi ya wastaafu wakati wa ziara yake ya kukagua utekelezaji wa maagizo ya Mhe.Rais  Dkt. John Magufuli kwa mifuko ya NSSF  na PSSSF.
Meneja wa Mfuko wa Hifadhi wa NSSF Tawi la Moshi Bi.Mary Onesmo akimuonesha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.Jenista Mhagama namna huduma zinavyotolewa katika madirisha ya kusikiliza wastaafu katika Ofisi hizo alipotembelea Januari 10, 2019.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi ya jamii NSSF Bw.William Erio (katikati) akieleza jambo kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.Jenista Mhagama wakati wa ziara yake katika Ofisi za NSSF Moshi.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.Jenista Mhagama akiangalia namna watumishi wa NSSF wanavyotoa huduma kwa wateja wao wakati wa ziara yake katika Ofisi hizo Moshi Mjini.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi ya jamii NSSF Bw.William Erio maelezo ya ufafanuzi kuhusu mifuko ya Hifadhi nchini kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.Jenista Mhagama alipotembelea Mfuko wa NSSF Moshi.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.Jenista Mhagama (wan ne kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watendaji wa Serikali pamoja na wale wa mifuko ya Hifadhi wakati wa ziara yake katika ofisi za Moshi mkoani Kilimanjaro.Kulia kwa Waziri ni Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Kippi Warioba na kushoto kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi ya jamii NSSF Bw.William Erio


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.