Monday, February 19, 2018

MAJALIWA AHITIMISHA ZIARA WILAYANI MISUNGWI

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua shamba la pamba lenye ukubwa w hekari 6 la  Bw. Muhoja Ngole (kulia kwa Waziri Mkuu) katika kijiji cha Mondo wilayani Misungwi, Februari 19, 2018.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwapungia wananchi wa kijiji cha Nyamanyinza wilayani Misungwi wakati alipowasili kwenye uwanja wa michezo kuhutubia mkutano wa hadhara kijijini hapo, Februari 19, 2018.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikata utepe wakati alipoweka jiwe la msingi la mradi wa maji wa Mbarika – Misasi katika  kijiji cha Manawa  wilayani Misungwi, Februari 19, 2018. Wa pili kulia  ni mbunge wa Misungwi, Charles Kitwanga na wa pili kushoto ni Mkuu wa mkoa  wa Mwanza, John Mongella.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiweka jiwe la msingi la mradi wa maji wa Mbarika- Misasi katika kijiji cha Manawa wilayani Misungwi Februari 19, 2018. Wapili kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Mwanza, John Mongella na wa pili kulia ni Mbunge wa Misungwi, Charles Kiwanga.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akikagua  madarasa yanayojengwa kwa nguvu za wananchi katika kijiji cha Nyamayinza wilayani Misungwi Februari 19, 2018. Kushoto ni Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angelina Mabula, wa pili kulia ni Mbunge wa Misungwi, Charles Kitwanga na wa tatu kulia ni Mkuu wa wilaya ya Misungwi, Juma Sweda.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akihutubia mkutano wa hadhara katika kijiji cha Nyamayinza wilayani Misungwi, Februari 19, 2018.



EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.