Saturday, February 17, 2018

WAZIRI MKUU AKIWA UKEREWE NA BUNDA

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima wakizungumza na Noella Tekela, mwanafunzi wa darasa la sita katika  shule ya msingi ya Masaunga wilayani Bunda baada ya kuwahutubia wavuvi, wafanyabiashara wa samaki na wananchi  kwenye kijiji cha Kisorya  Februari 17, 2018. Mtoto huyo alionekana akiandika kwa usahihi katika daftari hotuba yote ya Waziri Mkuu katika mkutano huo.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mmiliki wa Pantoni ya MV Nyehunge, Said Mohammed  kwenye gati la Kirumba wakati aliposafiri  na chombo hicho kutoka jijini Mwanza kwenda Ukerewe Februari 18, 2018.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na wafanyakazi wa Pantoni ya MV Nyehunge  kwenye gati la Kirumba wakati aliposafiri na chombo hicho kutoka jijini Mwanza kwenda Ukerewe Februari 18, 2018.


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.