Friday, February 16, 2018

IDARA YA URATIBU WA SHUGHULI ZA SERIKALI YAENDESHA KIKAO CHA TATHIMINI NA UFUATILIAJI JUU YA UKATILI DHIDI YA WANAWAKE NA WATOTO.

Mwenyekiti wa kikao cha Kujadili Rasimu ya Mpango wa Tathimini na Ufuatiliaji wa Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto kwa miaka mitano  2017/18-2021/22 Bw.Joseph Kiraia akichangia hoja wakati wa kikao hicho kilichoratibiwa na Idara ya Uratibu wa Shughuli za Serikali Ofisi ya Waziri Mkuu Februari 16, 2018. 

Mshauri Mwelekezi wa Mambo ya Tathimini na Ufuatiliaji Bw.Luhuvilo Sanga aliwasilisha mada wakati wa kujadili Rasimu ya Mpango wa Tathimini na Ufuatiliaji wa Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto kwa miaka mitano   katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Waziri Mkuu Dodoma.

Mtendaji Mkuu wa Mtandao wa Malezi, Makuzi, Maendeleo ya Watoto Wadogo Tanzania Bw.Bruno Ghumpi akiuliza swali wakati wa kikao cha kujadili Rasimu ya Mpango wa Tathimini na Ufuatiliaji wa Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto kilichoandaliwa na Idara ya Uratibu wa Shughuli za Serikali Ofisi ya Waziri Mkuu Februari 16, 2018

Mchambuzi wa Masuala ya Sera Bw. Ezekiel Swema akitoa maelezo kwa baadhi ya wanakikundi cha Kujadili Rasimu ya Mpango wa Tathimini na Ufuatiliaji wa Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto wakati wa kikao hicho.

Mtendaji Mkuu wa Mtandao wa Malezi, Makuzi, Maendeleo ya Watoto Wadogo Tanzania Bw.Bruno Ghumpi akichangia hoja wakati wa kazi za vikundi ili kujadili Rasimu ya Mpango wa Tathimini na Ufuatiliaji wa Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto.

Afisa Kazi Mwandamizi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu) Bi. Pendo Berege akichangia hoja wakati wa kikao cha kujadili Rasimu ya Mpango wa Tathimini na Ufuatiliaji wa Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto kilichofanyika Ukumbi wa mikutano Ofisi ya Waziri Mkuu Dodoma.


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.