Thursday, March 7, 2019

WATUMISHI OFISI YA WAZIRI MKUU WAPANDA MITI 250 KATIKA OFISI ZAO MPYA IHUMWA DODOMA.

Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu, Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Nigel Msangi akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watumishi wa ofisi yake nje ya jengo jipya la ofisi hiyo linaloendelea kujengwa katika Mji wa Serikali Ihumwa Dodoma.
Baadhi ya watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakiosha mikono mara baada ya zoezi la kupanda miti katika eneo la Ofisi zao mpya katika Mji wa Serikali Ihumwa Dodoma.
Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu, Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Nigel Msangi (katikati mwenye shati lenye madoa meupe na meusi) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watumishi wa Ofisi hiyo mara baada ya zoezi la kupanda miti katika Ofisi zao mpya Ihumwa Dodoma.
Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Uratibu wa Maafa (Mipango na Utafiti) Bw.Bashiru Taratibu akipanda mti katika zoezi la upandaji miti 250 katika Ofisi yao mpya Ihumwa Dodoma.
Sehemu ya watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakipanda miti aina ya Midodoma katika eneo la Ofisi zao katika Mji wa Serikali Ihumwa Dodoma Machi 7, 2019.
Mtaalam wa masuala ya misitu kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii Bw.Chambo akionesha moja ya miti aina ya midodoma kwa watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu walioshiriki katika zoezi la upandaji miti 250 katika ofisi zao mpya zinazoendelea kujengwa katika Mji wa Serikali Ihumwa Dodoma.
Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu, Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Nigel Msangi akizungumza na watumishi wa Ofisi yake wakati wa zoezi la upandaji wa miti 250 katika eneo la ofisi yao mpya katika Mji wa Serikali Ihumwa Dodoma Machi 7, 2019.
Afisa Mwandamizi (Utawala na Itifaki) Idara ya Maadhimisho na Sherehe za Taifa Ofisi ya Waziri Mkuu Bw.Steven Magoha akipanda mti wakati wa zoezi hilo.
Msaidizi wa Ofisi Idara ya Uratibu wa shughuli za Serikali Ofisi ya Waziri Mkuu Bi.Zuhura Omari akipanda mti wakati wa zoezi hilo.
Afisa Mwandamizi (Utawala na Itifaki) Idara ya Maadhimisho na Sherehe za Taifa Ofisi ya Waziri Mkuu Bi Isabela Katondo akipanda mti wakati wa zoezi hilo.
Kaimu Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Sekta Binafsi Bw.Vedastus Manumbu akishiriki zoezi la kupanda miti katika eneo la jengo la Ofisi ya Waziri Mkuu Ihumwa Dodoma


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.