Monday, March 18, 2019

WAZIRI MHAGAMA AWAFUNDA WATUMISHI WA OFISI YA WAZIRI MKUU.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akihutubia watumishi wa Ofisi yake walioshiriki katika mkutano wa baraza la wafanyakazi la ofisi hiyo uliofanyika Machi 18, 2019 katika Ukumbi wa mikutano wa ofisi hiyo Jijini Dodoma.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Uwekezaji Mhe.Angellah Kairuki akizungumza jambo wakati wa kikao cha baraza la wafanyakazi la ofisi hiyo Machi 18, 2019 Jijini Dodoma.
Mawaziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Mhe.Jenista Mhagama anayeshughulikia Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu pamoja na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu(Uwekezaji) Mhe. Angellah Kairuki wakiimba wimbo wa umoja na mshikamano wakati wa mkutano huo.
Sehemu ya wajumbe wa baraza la wafanyakazi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakiimba wimbo wa Umoja na Mshikamano wakati wa mkutano huo.
Sehemu ya wajumbe wa baraza la wafanyakazi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakifuatilia ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu Ofisi hiyo, anayeshughulikia Bunge na Waziri Mkuu Bi.Maimuna Tarishi wakati wa kikao hicho.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akimkabidhi Katibu mpya wa Baraza la Wafanyakazi wa ofisi hiyo Bw.Pascal Vyagusa nyaraka za utendaji kazi katika nafasi hiyo mara baada ya kuteuliwa na wajumbe wa baraza hilo.
Mkurugenzi wa Sera na Mipango Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Packshard Mkongwa. akiwasilisha Taarifa ya Utekelezaji wa Mpango wa Bajeti ya Ofisi hiyo kwa mwaka wa fedha 2018/2019 na Mpango na Makadirio ya Bajeti ya Mwaka 2019/2020 wakati wa kikao hicho.
Mmoja wa wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi Ofisi ya Waziri Mkuu Bi. Amina Simbaulanga akichangia jambo wakati wa kikao hicho.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama pamoja na Waziri wa Nchi ofisi hiyo anayeshughulikia Uwekezaji Mhe. Angella Kairuki wakikata utepe nyaraka za utendaji kazi kwa viongozi wa baraza la wafanyakazi wa ofisi hiyo wakati wa mkutano wa baraza lao.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama (katikati) pamoja na Waziri wa Nchi Ofisi hiyo anayeshughulikia Uwekezaji Mhe. Angellah Kairuki (mwenye koti jeusi) wakiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa baraza la wafanyakazi la ofisi hiyo mara baada ya ufunguzi wa kikao chao kilichofanyika Machi 18, 2019.


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.