Wednesday, July 31, 2019

SERIKALI YAANZA KUPIMA UTAYARI WA KUKABILI EBOLA MIPAKA YA KAGERA



Mkurugenzi Msaidizi (Utafiti na Mipango) Idara ya Menejimenti ya Maafa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Bashiru Taratibu akieleza umuhimu wa menejimenti ya maafa ya magonjwa ya mlipuko, wakati wa ufunguzi wa zoezi la kupima  utayari wa kukabili Ugonjwa wa Ebola kwa watoa huduma za afya Mkoani Kagera (hawapo pichani) tarehe 30 Julai, 2019, mjini Bukoba mkoani Kagera.


Na. OWM, KAGERA

Serikali kupitia uratibu wa Ofisi ya Waziri Mkuu imezindua zoezi la  kupima utayari wa kukabili  mlipuko wa ugonjwa wa Ebola ili kupima utayari wa sekta na wadau mbalimbali, ikiwemo jamii  katika kukabili mlipuko wa ugonjwa huo katika maeneo ya mipakani.

Akiongea wakati wa kuzindua zoezi  hilo la siku tano jana, tarehe  30 Julai 2019, mjini Bukoba,   mkoani Kagera, Katibu Tawala wa mkoa huo, Profesa Faustin Kamuzora aliwataka wananchi kuchukua tahadhari kwa kujielimisha kuhusu ugonjwa wa Ebola na kusisitiza ni muhimu  kuchukua tahadhari kwa kuwa hadi sasa hakuna mgonjwa aliyegundulika kuwa na dalili za Ebola  hapa nchini Tanzania.

“Tunapaswa kufanya juhudi kubwa ili kama ambavyo hadi hivi sasa hakuna mgonjwa wa Ebola nchini kwetu, basi tuendelee kuwa salama, kwa kuwa faida zake ni kubwa kuliko kupambana na mlipuko,” alisema Prof. Kamuzora.

Aidha, Profesa. Kamuzora aliongeza kuwa Uratibu  wa sekta za Afya na sekta zingine  katika kukabili  na Ebola ni muhimu sana hususani  kwenye kukabili na magonjwa ya mlipuko. Alifafanua kuwa ugonjwa kama Ebola si suala la kiafya tu, ni suala la jamii na sekta zote hivyo iwapo idara zote husika kama vile  uhamiaji, afya, serikali za mitaa zikifanya kazi zake vyema haitakuwa vigumu kuwagundua wenye dalili na kuchukua tahadhari stahiki.

Awali akiongea wakati wa Uzinduzi wa zoezi hilo Mkurugenzi Msaidizi (Utafiti na Mipango), Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Bashiru Taratibu alisema juhudi zinapaswa kufanyika ili ugonjwa wa Ebola usiingie nchini na kusababisha maafa ya ugonjwa wa mlipuko.

“Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya menejimenti ya maafa itaendelea kufanya kadri inavyowezekana maafa ya ugonjwa wa mlipuko yasitokee, na ikishindikana basi kupunguza athari zake.  Ndio maana malengo ya zoezi hili ni kupima utayari wa kukabili ugonjwa wa Ebola na hatimaye tuweze  kujenga utayari wetu,” alisema,  Taratibu.
Akiongea wakati wa uzinduzi  wa zoezi hilo, Mratibu wa zoezi hilo kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt.  Faraja Msemwa amefafanua kuwa watoa huduma za afya na sekta zingine watakuwa wakifanya zoezi  kwa namna ambavyo itakuwa  iwapo mtu mwenye Ebola atapatikana mahali fulani katika jamii.

“Watu watakaochukua nafasi ya ‘wagonjwa’’ wakati wa zoezi hili si wagonjwa halisi wa Ebola, lakini shughuli zote zitakazofanyika wakati wa zoezi la utayari zitaakisi mazingira halisi toka nchi ambazo zimewahi kukabiliwa na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola” alisisitiza Dkt. Msemwa.

Dkt. Msemwa aliongeza kuwa pamoja na kuwa zoezi hilo kuwa  litafanyika kwa mkoa wa Kagera na Kigoma, Aidha,  mikoa mingine ambayo Ipo hatarini kwa mlipuko wa ugonjwa wa Ebola ni pamoja na Mbeya, Songwe, Katavi, Rukwa, Dar es salaam, Mwanza na Dodoma.

Aidha, Dkt. Msemwa ali tishio la ugonjwa wa Ebola nchini Tanzania linatokana na mlipuko wa ugonjwa huo kwenye jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) tangu Agosti mwaka jana.  Kwa kuzingatia Mkoa wa Kagera unapaka na nchi ya Rwanda na Uganda

Kwa mujibu wa taarifa toka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto zinaeleleza kuwa tishio la ugonjwa wa Ebola nchini Tanzania linatokana na mlipuko wa ugonjwa huo kwenye jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) tangu Agosti mwaka jana ambapo  hadi kufikia Julai 23    mwaka huu jumla ya wananchi wa DRC, 2612 walidhihirika kuambukizwa ugonjwa wa Ebola na  kulikuwapo na vifo 1,756.

Zoezi hilo linaratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa ushirikiano na wadau wa maendeleo. Mazoezi hayo  yatafanyika kati ya tarehe 30 Julai na tarehe 8 Agosti mwaka 2019 katika vituo vya kutolea huduma za afya na maeneo ya mipaka mkoani Kagera na Kigoma.

MWISHO


 Katibu Tawala Mkoa wa Kagera Prof. Faustin Kamuzora akisisitiza kuchukua tahadahari kwa ugonjwa wa Ebola usiingie nchini wakati wa akifungua zoezi la kupima  utayari wa kukabili Ugonjwa wa Ebola kwa watoa huduma za afya Mkoani Kagera (hawapo pichani) tarehe 30 Julai, 2019, mjini Bukoba mkoani Kagera.
Mwakilishi kutoka Shirika la Afya Duniani Dkt. Refeya Ndyamuba akifafanua jambo kwa Katibu Tawala Mkoa wa Kagera Prof. Faustin Kamuzora wakati wa akifungua zoezi la kupima  utayari wa kukabili Ugonjwa wa Ebola kwa watoa huduma za afya Mkoani Kagera (hawapo pichani) tarehe 30 Julai, 2019, mjini Bukoba mkoani Kagera, kulia ni Mkurugenzi Msaidizi (Utafiti na Mipango) Idara ya Menejimenti ya Maafa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Bashiru Taratibu
Baadhi ya wawezeshaji  wa zoezi la kupima  utayari wa kukabili Ugonjwa wa Ebola mkoani Kagera,  wakijadiliana namna ya kuendesha zoezi hilo ,tarehe 31 Julai, 2019.
Baadhi ya wawezeshaji  wa zoezi la kupima  utayari wa kukabili Ugonjwa wa Ebola mkoani Kagera,  wakijadiliana namna ya kuendesha zoezi hilo ,tarehe 31 Julai, 2019.
Baadhi ya wawezeshaji  wa zoezi la kupima  utayari wa kukabili Ugonjwa wa Ebola mkoani Kagera,  wakijadiliana namna ya kuendesha zoezi hilo ,tarehe 31 Julai, 2019.


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.