Saturday, July 27, 2019

NAIBU WAZIRI MAVUNDE AWATAKA VIJANA KUENZI MCHANGO WA BABA WA TAIFA

Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Vijana na Ajira Mhe. Anthony Mavunde akizungumza na Viongozi, Watumishi wa Hifadhi ya Mlima Kilimanjaro na wakazi wa Marangu wakati wa hafla fupi ya kuwaaga vijana watakaopanda Mlima Kilimanjaro ikiwa ni ishara ya kumbukizi ya miaka 20 ya Kifo cha Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere.

Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Mhe. Kippi Warioba akielezea jambo kwa vijana 8 walioshiriki katika shughuli hiyo ya kupanda Mlima Kilimanjaro ikiwa ni kuadhimisha kumbukizi ya miaka 20 ya Kifo cha Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere. Kushoto ni Mkurugenzi wa Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo kutoka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Bi. Mwanaidi Ali.
Baadhi ya Watumishi wa Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro wakimsikiliza Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana na Ajira) Mhe. Anthony Mavunde (hayupo pichani) wakati wa hafla ya kuwaaga vijana hao.
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana na Ajira) Mhe. Anthony Mavunde akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro kwa ajili ya kuwaaga vijana kutoka Mkoa wa Songwe, Arusha, Tanga, Kaskazini Unguja na Kusini Unguja kabla ya kupanda Mlima huo.
Kamishna Mwandamizi wa Kanda ya Kaskazini, Herman Batiho akimfafanulia Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana na Ajira) Mhe. Anthony Mavunde (kulia) kuhusu hifadhi ya Mlima Kilimanjaro, alipowasilia Mkoani huo kwa lengo la kuwaaga vijana hao.
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Vijana Bw. James Kajugusi akielezea kuhusu vijana watakaopanda Mlima Kilimanjaro kwa awamu ya pili ikiwa ni ishara ya kumbukizi ya Miaka 20 ya Kifo cha Baba wa Taifa Mwl. Julius K. Nyerere. Kushoto ni Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana na Ajira) Mhe. Anthony Mavunde.
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana na Ajira) Mhe. Anthony Mavunde (kulia) akijadili jambo na Kamishna Mwandamizi wa Kanda ya Kaskazini, Herman Batiho alipowasili katika hifadhi hiyo kwa lengo la kuwa kuwaaga vijana waliopanda Mlima Kilimanjaro kwa awamu ya pili.
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana na Ajira) Mhe. Anthony Mavunde (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na Viongozi na vijana watakaopanda Mlima Kilimanjaro, alipowasilia Mkoani huo kwa lengo la kuwaaga vijana hao.
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana na Ajira) Mhe. Anthony Mavunde akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Anna Mghirwa alipomtembelea ofisini kwake kabla ya kuelekea kwenye Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro.


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.