Saturday, June 22, 2019

KATIBU MKUU MASSAWE AHIMIZA USHIRIKIANO KWA WATUMISHI

Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Bw. Andrew Massawe akizungumza na Watumishi wa ofisi hiyo (hawapo pichani) alipokutana nao kujadili utendaji kazi ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma.

Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu wa Ofisi hiyo, Bw. Peter Kalonga akieleza jambo kwa watumishi wa Ofisi hiyo (hawapo pichani) ikiwa ni sehemu ya maaadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma.

Sehemu ya Wakuu wa Idara na Vitengo wa Ofisi hiyo wakifuatilia maelezo ya Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Bw. Andrew Massawe (hayupo pichani) walipokutana Jijini Dodoma.
Mmoja wa Watumishi wa Ofisi hiyo Bi. Grace Kigula akielezea baadhi ya changamoto wanazokumbana nazo katika utendaji walipokutana na Katibu Mkuu wa ofisi hiyo ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Bw. Andrew Massawe (katikati) akifafanua jambo kwa wadau (hawapo pichani) alipokutana nao kwa lengo la kujadiliana pamoja na kusikiliza maoni, ushauri na changamoto wanazokutana nazo ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma mwaka 2019. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu, Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) Bw. Johanes Majura na kulia ni Mwanasheria kutoka Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Bi. Suzan Ndomba.
Mmoja wa wadau kutoka Kampuni ya RECO Engineering Ltd, Bw. Abubakar Mukadam akichangia mada kuhusu masuala ya vibali vya kazi walipokutana na Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Bw. Andrew Massawe (haupo pichani) ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma.

Baadhi ya watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu wakimsikiliza kwa makini Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Andrew Massawe alipokutana nao kusikiliza maoni na changamoto wazokabiliana nazo katika utendaji kazi wao.
Naibu Katibu Mkuu, Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) Bw. Johanes Majura (kushoto) akifafanua jambo kuhusu masuala ya vyama vya wafanyakazi wakati wa mkutano huo uliofanyika ghorofa la PSSSF, Jijini Dodoma. Kulia ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Bw. Andrew Massawe.
Mwanasheria kutoka Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Bi. Suzan Ndomba akielezea kuhusu baadhi ya Sheria zinazowaongoza Waajiri nchini wakati wa kikao na Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Bw. Andrew Massawe (katikati) alipokutana na wadau mbalimbali wa ofisi hiyo. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu, Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) Bw. Johanes Majura

Baadhi ya wadau wakifuatilia maelezo ya Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Bw. Andrew Massawe (haupo pichani) walipokutana kujadili masuala mbalimbali kuhusu sekta ya Kazi, Maendeleo ya Vijana, Ajira, Huduma kwa Watu wenye Ulemavu, Hifadhi ya Jamii na masuala ya Vyama vya Wafanyakazi.
Sehemu ya ya wadau wakifuatilia maelezo ya Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Bw. Andrew Massawe (haupo pichani) walipokutana kujadili masuala mbalimbali kuhusu sekta ya Kazi, Maendeleo ya Vijana, Ajira, Huduma kwa Watu wenye Ulemavu, Hifadhi ya Jamii na masuala ya Vyama vya Wafanyakazi.




EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.