Thursday, June 13, 2019

DHANA YA AFYA MOJA YATUMIKA KUPIMA KWA VITENDO HATUA ZA USIMAMIZI NA UCHUNGUZI WA MAGONJWA YA MLIPUKO MPAKANI NAMANGA

Daktari katika mpaka wa Tanzania na Kenya kwenye eneo la Namanga, Anna Anthony, akiwapima wasafiri wanaopita katika mpaka huo, wakati wa zoezi la Kupima Utayari wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Kukabiliana na magonjwa ya mlipuko mipakani, leo  tarehe 13 Juni, 2019.

Na. OWM, NAMANGA.

Kufuatia zoezi linaloendelea mpakani mwa Tanzania na Kenya kwenye eneo la Namanga, ambalo linajikita katika Kupima Utayari wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Kukabiliana na magonjwa ya mlipuko mipakani, leo tarehe 13 Juni, 2019, Wataalamu wa sekta za Afya wa Tanzania na Kenya, katika makundi tofauti wameweza kutekeleza kwa vitendo kwa kutumia Dhana ya Afya moja katika  Kupima kwa vitendo hatua za kujiandaa na kukabili Ugonjwa wa Homa ya Bonde la Ufa.

Wataalam hao wameweza kutathmini uwezo wa uchunguzi na usimamizi wa wagonjwa wa Homa ya Bonde la Ufa mpakani, pamoja na kufanyia majaribio ya utekelezaji wa Mipango ya Dharura ya Taifa na Kanda, Miongozo ya Utendaji katika kukabili na kupunguza madhara ya ugonjwa wa Homa ya Bonde la Ufa kwa Wanyama na Binadamu.

Zoezi hilo, linazingatia Dhana ya Afya moja ambayo hujumuisha sekta ya afya ya binadamu, wanyamapori, mifugo na mazingira katika kujiandaa, kufuatilia na kukabili magonjwa yanayoathiri binadamu. 

MWISHO.


Askari Mpakani mwa Tanzania na Kenya kwenye eneo la Namanga akimwekea kwenye mikono Dawa ya kusafishia mikono msafiri aliyekuwa akipita katika mpaka huo wakati wa   zoezi la Kupima Utayari wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Kukabiliana na magonjwa ya mlipuko mipakani,  leo tarehe  13, Juni 2019.
Mtaalamu wa Afya akimhudumia  mmoja wa wasafiri waliokuwa wakipita katika mpaka wa Tanzania na Kenya, kwenye eneo la Namanga aliyeigiza kuugua,  wakati wa zoezi la Kupima Utayari wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Kukabiliana na magonjwa ya mlipuko mipakani, leo  tarehe 13 Juni, 2019.
Baadhi ya Wataalamu wa  Afya wakimhudumia  mmoja wa wasafiri waliokuwa wakipita katika mpaka wa Tanzania na Kenya, kwenye eneo la Namanga aliyeigiza kuugua,  wakati wa zoezi la Kupima Utayari wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Kukabiliana na magonjwa ya mlipuko mipakani, leo  tarehe 13 Juni, 2019.
Mtaalamu wa Afya akipata maelezo kutoka kwa ndugu wa    mmoja wa wasafiri waliokuwa wakipita katika mpaka wa Tanzania na Kenya, kwenye eneo la Namanga aliyeigiza kuugua,  wakati wa zoezi la Kupima Utayari wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Kukabiliana na magonjwa ya mlipuko mipakani, leo  tarehe 13 Juni, 2019
Mtaalamu wa Afya akinyunyizia dawa gari ambalo lilikuwa limewabeba abiria walioigiza  kuumwa wakati wakitaka kupita katika mpaka wa Tanzania na Kenya, kwenye eneo la Namanga,  wakati wa zoezi la Kupima Utayari wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Kukabiliana na magonjwa ya mlipuko mipakani, leo  tarehe 13 Juni, 2019.
Baadhi ya Wataalamu wa Afya  katika mpaka wa Tanzania na Kenya, kwenye eneo la Namanga wakivua nguo za kinga mara baada ya kuwahudumia wasafiri walioigiza kuumwa  wakati wakipita kwenye mpaka huo,  wakati wa zoezi la Kupima Utayari wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Kukabiliana na magonjwa ya mlipuko mipakani, leo  tarehe 13 Juni, 2019.


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.