WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewahakikishia
 wakulima wa korosho ambao bado hawajalipwa kuwa Serikali italipa fedha 
hizo ambazo ni zaidi ya bilioni 20 mwaka huu.
Amesema
 wakulima ambao bado hawajalipwa au kumaliziwa malipo yao baada ya 
Serikali kumaliza uhakiki majina yao yatapelekwa TADB kwa ajili ya 
malipo.
Waziri
 Mkuu ametoa kauli hiyo leo (Jumamosi, Juni 1, 2019) katika kikao cha 
Halmashauri Kuu ya CCM mkoa wa Lindi, kilichofanyika kwenye ukumbi wa 
CCM mkoa.
“Wakulima
 wote wanaodai malipo yao ya korosho watalipwa katika mwaka huu wa fedha
 kwa kuwa ni haki yao na kwamba Serikali haitodhulumu haki ya mkulima 
yeyote.”
Kadhalika,
 Waziri Mkuu amesisitiza suala la uboreshwaji wa miundombinu mbalimbali 
ya kutolea huduma zikiwemo barabara ili ziweze kupitika kwa urahisi 
wakati wote.
Amesema
 uboreshwaji wa mbiundombinu pamoja na huduma nyingine za jamii ni 
jukumu la watendaji, hivyo wahakikishe wananchi wote wanahudumiwa bila 
ya kubaguliwa.
“Kila
 aliyepewa jukumu ahakikishe analitekeleza ipasavyo. Watendaji 
hakikisheni mnawatumikia Watanzania wote vizuri, kusiwe na ubaguzi wa 
kisiasa, kidini na kikabila.”
Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Ilani katika kikao hicho, Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Godfrey Zambi amesema zoezi la malipo ya fedha za korosho zilizohakikiwa linaendele.
Amesema
 hadi Mei 31 mwaka huu kilo 51,990,999.97 zenye thamani ya sh. bilioni 
171,570,299,912 ambazo ni sawa na asilimia 87.6 zimeshalipwa kwa 
wakulima husika.
Mkuu
 huyo wa mkoa amesema kiasi cha bilioni 23,404,086,508 bado hazijalipwa 
kwa wakulima wa korosho wa mkoa wa Lindi. Korosho hizo zilihakikiwa 
kituo cha Mtwara.
Kikao
 hicho kimehudhuriwa na wabunge wa mkoa wa Lindi, Wakuu wa Wilaya, 
Wakurugenzi wa Halmashauri na Manispaa pamoja na Wakuu wa Idara.
 
 
 
 
EmoticonEmoticon
Note: Only a member of this blog may post a comment.