*Ni baada ya kutoa sehemu ya eneo lake kwa ajili ya ujenzi wa shule
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameushukuru
 uongozi wa Kanisa Katoliki Jimbo la Lindi kwa kutoa sehemu ya eneo lake
 na baadhi ya majengo kwa ajili ya ujenzi wa shule.
Jimbo
 Katoliki la Lindi limetoa eneo hilo lilipo katika Parokia ya Mnacho 
wilayani Ruangwa ambalo awali ilikuwa shule ya msingi ya Mnacho sasa 
imebadilishwa na kuwa sekondari.
Waziri
 Mkuu ametoa shukurani hizo leo (Jumapili, Juni 2, 2019) alipokwenda 
kwenye kanisa Katoliki la Theresia wa Mtoto Yesu, Parokia ya Mnacho 
kuwasalimia waumini.
Amesema
 lengo la kuibadilisha shule hiyo kuwa Shule ya Sekondari ya Wasichana 
ya Lucas Malia ni kuwawezesha watoto wa kike wa Wilaya hiyo kusoma 
katika mazingira mazuri.
Waziri
 Mkuu ambaye ameambatana na Mkewe Mary amesema shule hiyo ya bweni 
itawapunguzia vishawishi watoto wa kike, hivyo kuwawezesha kutimiza 
malengo yao. 
Awali,
 uongozi wa Parokia hiyo uliipongeza Serikali ya Awamu ya Tano kwa 
kuboresha huduma za jamii zikiwemo za afya, elimu pamoja na miundombinu 
katika wilaya hiyo.
Naye,
 Mkuu wa wilaya ya Ruangwa, Hashim Mgandilwa amewaomba viongozi wa dini 
washikamane na wahakikishe wanatatua changamoto ya mmomonyoko wa 
maadili.
Amesema
 changamoto ya mmomonyoko wa maadiji katika jamii hususani kwa vijana ni
 kubwa, hivyo ni jukumu lao kuhakikisha kwamba wanawarejesha kwenye 
maadili bora.
Kadhalika,
 Waziri Mkuu amekagua ujenzi wa shule ya Sekondari ya Wasichana ya Lucas
 Malia na amesema kwamba ameridhishwa na maendeleo ya ujenzi wake.
Shughuli
 zinazoendelea katika shule hiyo ni pamoja na ujenzi wa mabweni, vyumba 
vya madarasa, maabara na nyumba nne za walimu ambazo tayari ujenzi wake 
umekamilika.
EmoticonEmoticon
Note: Only a member of this blog may post a comment.