Sunday, June 2, 2019

WAZIRI MHAGAMA AZINDUA BARAZA LA TAIFA LA USHAURI KWA WATU WENYE ULEMAVU

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akizungumza na wajumbe wa Baraza jipya la Taifa la ushauri kwa Watu wenye Ulemavu (hawapo pichani) kuhusu umuhimu wa baraza hilo kushirikiana na Serikali wakati akizindua Baraza hilo katika ukumbi wa mikutano wa PSSSF, Jijini Dodoma.
Naibu Waziri,Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika masuala ya Watu wenye Ulemavu Mhe. Stella Ikupa akielezea jambo kwa wajumbe wa Baraza wakati wa uzinduzi wa Baraza hilo uliofanyika tarehe 2 Juni, 2019 Jijini Dodoma.
Mwenyekiti mpya wa Baraza la Taifa la ushauri kwa Watu wenye Ulemavu Dkt. Lukas Kija akitoa neno la shukrani kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama wa pili kutoka kulia na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika masuala ya Watu wenye Ulemavu Mhe. Stella Ikupa wa pili kutoka kushoto mara baada ya kuzinduliwa kwa Baraza hilo. Kushoto ni Katibu Mkuu wa ofisi hiyo Bw. Andrew Massawe.
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Bw. Andrew Massawe akifafanua jambo kwa wajumbe wa Baraza hilo (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa Baraza hilo uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa PSSSF, Juni 2, 2019 Jijini Dodoma.
Baadhi ya wajumbe wa Baraza hilo wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama (hayupo pichani).
Sehemu ya wajumbe wa Baraza hilo wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama (hayupo pichani) wakati akizindua Baraza hilo Jijini Dodoma.
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha huduma kwa Watu wenye Ulemavu Bi. Josephine Lyengi akielezea jinsi kitengo hicho kinavyohudumia Watu wenye Ulemavu.
Mkalimani wa lugha za alama Bw. Baster Mlawa (kulia) akimfafanulia Mwenyekiti Chama cha Viziwi Tanzania Bw. Nedrosy Mlawa wa pili kutoka kulia (wenye uziwi) kuhusu maelezo yaliyokuwa yakitolewa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama (hayupo pichani).
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akitoa mkono wa pongezi kwa Mwenyekiti mpya wa Baraza la Taifa la ushauri kwa Watu wenye Ulemavu Dkt. Lukas Kija wakati wa hafla ya kuzindua Baraza hilo, Jijini Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akisalimiana na baadhi ya wajumbe wakati wa hafla ya uzinduzi wa Baraza jipya la Taifa la ushauri kwa Watu wenye Ulemavu.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akiwa kwenye picha ya pamoja na wajumbe wa Baraza jipya la Taifa la ushauri kwa Watu wenye Ulemavu mara baada ya kuzindua Baraza hilo Jijini Dodoma. Wa pili kutoka kulia ni Mwenyekiti mpya wa Baraza la Taifa la ushauri kwa Watu wenye Ulemavu Dkt. Lukas Kija, wa pili kutoka kushoto ni Naibu Waziri,Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika masuala ya Watu wenye Ulemavu Mhe. Stella Ikupa. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Andrew Massawe na kulia ni Katibu Taifa wa Shirikisho la Vyama vya Watu wenye Ulemavu (SHIVYAWATA) Bw. Jonas Lubayo.


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.