Wednesday, August 28, 2019

MAJALIWA AKUTANA NA WAZIRI MKUU WA MAURITIUS, PRAVIND KUMAR

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Waziri Mkuu wa Mauritius, Pravind Kumar kabla ya mazungumzo yao  kwenye  Ukumbi wa Maonyesho wa Pacifico Yokohama nchini Japan, Agosti 28, 2019. Wote wawili wako Japan kuhudhuria Mkutano wa  Saba wa Tokyo International Conference on Africa Development -TICAD 7.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akizungumza na Waziri Mkuu wa Mauritius, Pravind Kumar kwenye ukumbi wa Maonyesho wa Pacifico Yokohama nchini Japan, Agosti 28, 2019. Wate wawili wanahudhuria Mkutano wa Saba wa Tokyo International Conference on Africa – TICAD 7.  Kushoto ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akizungumza na Waziri Mkuu wa Mauritius, Pravind Kumar kwenye ukumbi wa Maonyesho wa Pacifico Yokohama nchini Japan, Agosti 28, 2019. Wate wawili wanahudhuria Mkutano wa Saba wa Tokyo International Conference on Africa – TICAD 7.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi (wa pili kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na maofisa kutoka Ubalozi wa Tanzania nchini Japan,   Hifadhi za Taifa Tanzania(TANAPA) na Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) wakati alipotembelea banda la maonyesho la Tanzania kwenye Ukumbi wa Maonyesho wa Pacifico Yokohama nchini Japan, Agosti 28, 2019.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na maofisa kutoka Ubalozi wa Tanzania nchini Japan,   Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) na Bodi ya Utalii Tanzania  (TTB) wakati alipotembelea  banda la maonyesho la Tanzania kwenye Ukumbi wa Maonyesho wa Pacifico Yokohama nchini Japan, Agosti 28, 2019.



EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.