Tuesday, August 27, 2019

MAJALIWA ATEMBELEA KIWANDA CHA KUTENGENEZA MITAMBO YA UMEME CHA TOSHIBA NA MAKUMBUSHO YA SAYANSI YA KAMPUNI HIYO NCHINI JAPAN

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa Bibi Ririko Tanabe kuhusu historia ya kampuni ya Toshiba ya Japan wakati alipotembelea makumbusho ya Sayansi ya kampuni hiyo, Agosti 27, 2019 .
Waziri Mkuu, Kassim Majliwa akipata maelezo kutoka kwa  Bibi Ririko Tanabe   kuhusu redio ya kwanza  ilitengenezwa na kampuni ya Toshiba kwenye miaka ya 1930, wakati alipotembelea Makumbusho ya Sayansi ya Kampuni ya Toshiba nchini Japan, Agosti 27, 2019.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa  Bibi Ririko Tanabe   kuhusu redio ya kwanza ya kucheza santuri iliyotengenezwa na kampuni ya Toshiba kwenye miaka ya 1930, wakati alipotembelea Makumbusho ya Sayansi ya kampuni ya Toshiba nchini Japan, Agosti 27, 2019.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na ujumbe wake wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi na watumishi wa Makumbusho ya Sayansi ya Kampuni ya kampuni ya Toshiba nchini Japan baada ya kutembelea makumbusho hiyo, Agosti 27, 2019.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na viongozi wa kiwanda cha kutengeneza mitambo ya  kuzalisha umeme cha Tsurumi kinachomilikiwa na kampuni ya Toshiba nchini Japan wakati alipotembelea kiwanda hicho, Agosti 27, 2019. Kushoto ni Kaimu Balozi wa Tanzania nchini Japan, John Kambona.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na ujumbe wake wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi na wafanyakazi wa Kiwanda cha kutengeneza mitambo ya kuzalisha umeme cha Tsurumi kinachomilikiwa na kampuni ya Toshiba nchini Japan baada ya kutembelea kiwanda hicho, Agosti 27, 2019.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama chombo muhimu kinaunda  mitambo ya kuzalisha umeme wa maji na gesi (turbine) wakati alipotembelea kiwanda cha kutengeneza mitambo ya kuzalisha umeme cha Tsurumi kinachomilikiwa na Kampuni ya  Toshiba nchini Japan, Agosti 27, 2019. Wapili kulia ni Meneja Mkuu wa kiwanda hicho, Shinya Fujitsuka.



EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.