Saturday, August 10, 2019

VIJANA MKOANI RUVUMA WACHANGAMKIA FURSA YA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI

Katibu Mtendaji wa Balaza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) Bi. Beng’I Issa akizungumza na Vijana wa Mkoa wa Ruvuma kuhusu Programu ya Mafunzo ya Ujasiriamali na Usimamizi wa Biashara wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo katika Mkoa wa Ruvuma, Agosti 10, 2019.
Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma Bw. Hakimu Mafuru akizungumza na vijana walioshiriki katika mafunzo hayo ya ujasiriamali yaliyofanyika katika mkoa huo. (Kulia) ni Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Bw. Philliph Beno.
Baadhi ya vijana wanaojishughulisha na shughuli za kiuchumi wakifuatilia maelezo ya Katibu Mtendaji wa Balaza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) Bi. Beng’I Issa (hayupo pichani) alipokuwa akielezea kuhusu Programu ya Mafunzo ya Ujasiriamali.
Sehemu ya wajasiriamali wanaomiliki biashara wakifuatailia maelezo ya Katibu Mtendaji wa Balaza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) Bi. Beng’I Issa (hayupo pichani) alipokuwa akifungua mafunzo hayo katika mkoa huo.
Meneja wa Ufuatiliaji na Tathmini Bi. Flora Kajela akielezea kuhusu malengo ya Programu ya Mafunzo ya Ujasiriamali wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo yaliyofanyika katika Mkoa wa Ruvuma.
Mchumi Mkuu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Bw. Daudi Sailasi akielezea kuhusu programu ya kuongeza ujuzi kwa vijana inayoratibiwa na ofisi hiyo wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya Ujasiriamali na Usimamizi wa Biashara yaliyofanyika katika Mkoa huo. (Kulia) ni Katibu Mtendaji wa Balaza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) Bi. Beng’I Issa.
Mwezeshaji kutoka Balaza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC), Bw. Lucas Mafuru akitoa mada kuhusu uchambuzi wa ushindani na mikakati ya masoko kwa wajasiriamali (hawapo pichani).
Afisa Maendeleo ya Vijana kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Bw. Eliakim Mtawa akitoa mada kuhusu vihatarishi vya biashara na namna ya kuvikabili kwa wajasiriamali walioshiriki mafunzo hayo.
Mmoja wa Wajasiriamali Bw. Richard Mpangala akielezea kuhusu mbinu anazotumia kuendesha biashara yake alipokua amejifunza kuhusu masuala ya mapato na matumizi katika usimamizi wa biashara.
Bi. Pudencia Msangawale akionesha bidhaa anazotengeza na akielezea mbinu anazotumia kutafuta masoko ya bidhaa zake katika eneo lake la biashara.
Katibu Mtendaji wa Balaza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) Bi. Beng’I Issa (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na wajasiriamali walioshiriki mafunzo hayo ya ujasiriamali na usimamizi wa biashara.


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.