WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ameunda tume maalumu kwa ajili ya kufanya uchunguzi ili kubaini chanzo cha ajali
 ya moto iliyosababisha vifo vya watu zaidi ya 69 hadi mchana huu na 
wengine 70 kujeruhiwa wakati wakichota mafuta yaliyokuwa yakimwagika 
baada ya lori la mafuta kupinduka, mjini Morogoro.
“Hii
 tume inaanza kazi leo (Jumapili, Agosti 11, 2019), Hadi ijumaa inipe 
taarifa yake na hata kama mimi sijawajibika initaje. Ajali ya namna hii 
si mara ya kwanza ilitokea Mbeya eneo la Mbalizi. Naomba niwasihi 
Watanzani pale gari linapoanguka tusitume kama fursa twende tukaokoe 
binadamu waliopo pale”.
Waziri
 Mkuu ameunda tume hiyo leo (Jumapili, Agosti 11, 2019), wakati 
akizungumza na waombolezaji waliofika katika hospitali ya Mkoa wa 
Morogoro kwa ajili ya kutambua miili ya ndugu zao. Niko mbele yenu 
nikimwakilisha Rais Dkt. John Magufuli aliyenituma kuja kuungana nanyi 
kwenye siku hii ya huzuni”.
Waziri
 Mkuu amesema lazima wajiridhishe kama Serikali ilitekeleza vizuri 
jukumu lake kwa sababu ajali imetokea saa mbili asubuhi katikati ya mji,
 hivyo tunataka kujua ajalj ilipotokea kila mmoja alitumiza jukumu lake.
Amesema
 ajali imetokea karibu na Kituo Kikuu cha Mabasi na kuna polisi sasa je 
hawa wananchi waliopata ajali walienda na madumu ya kuchotea mafuta 
inamaana waliamka asubuhi wakijua ajali itatokea. “Najua pale ajali 
inapotokea trafiki wana wahi haraka hata kama kwa gari la kukodi. Watu 
walikuja na madumu, wengine kuchomoa betri nani aliwazuia.Je lilipoanza kuungua gari la zima moto lilikuja kwa wakati gani”.
Waziri
 Mkuu amesema lazima wajiridhishe ndani ya Serikali kama wamewajibika. 
“Kuna vitu vingi lazima tuviangalie tujue nani hakutimiza majukumu yake.
 Nadhani ujumbe mnaupata si vyema tutakimbilia vitu badala ya watu. 
Tunasikitika sana kwa yaliyotukuta hata upande wa Serikali tunasikitika 
kuwapoteza Watanzania”.
Pia,
 Waziri Mkuu amezungumzia kuhusu jitihada za kuokoa waliopata majeraha 
kwamba zinaendelea vizuri na jukumu lao kubwa kuwaombea marehemu 
wapumzike kwa amani na pia wawaombee wajeruhi waweze kupona.
Waziri
 Mkuu ameongeza kuwa, Rais Dkt. Magufuli tayari ameshatoa kibali cha 
kutolewa fedha kwa ajili ya kununuliwa vifaa tiba na dawa 
zinazohitajika.
Akizungumzia
 kuhusu idadi ya vifo na majeruhi waliotokana na ajali hiyo ambayo 
inatangazwa kupitia vyombo mvalimvali vya habari, Waziri Mkuu amesema ni
 vema takwimu hizo wakaacha zikatolewa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Bw. 
Stephen Kebwe.
“Kwenye
 vyombo vya habari tuelewane kwenye takwimu za vifo na majeruhi. Msiseme
 suala la takwimu anayetoa ni Mkuu wa Mkoa na matukio haya yapo chini 
yake. Nimeamua kusema hivi hizi takwimu zikitajwa nyinginyingi mnajenga 
hofu na taharuki kwa wananchi. Hili halikubaliki mkitaka taarifa 
mtafuteni mkuu wa mkoa”.
 Wakati Huo huo,
 amesema Rais Dkt. Magufuli alipokea taarifa mapema ya ajali ya lori la 
mafuta na kusababisha vifo vya Watanzania 69, ambapo alimtaka aende 
mkoani Morogoro kwa ajili ya kuwasilisha salamu za pole kwa wananchi wa 
Morogoro na Tanzania kwa ujumla kufuati tukio hilo la kuhuzunisha.
Waziri
 Mkuu amesema Rais Dkt. Magufuli anawaombea marehemu na majeruhi lakini 
pia amawataka wafiwa na wananchi wote wawe watulivu katika kipindi hiki 
kigumu cha kuondokewa na wapendwa wao.
“Mheshimiwa
 Rais amehuzunishwa sana na msiba huu ndio maana amenituma nilete ujumbe
 huu kwenu.Lakini pia nimekuja na salamu za pole kutoka kwa Makamu wa 
Rais, Mama Samia Suluhu Hassan. Jambo hili si dogo ni kubwa kwani 
tumepoteza ndugu zetu wengi. Kwa idadi hii kubwa ya ndugu zetu 
waliotangulia mbele za haki na wale waliopo kwenye maumivu si jambo la 
faraja”.
Waziri
 Mkuu amesema wananchi wasipeleke miili kwanza makaburini ili waweze 
kupitia na kutambua ndugu na rafiki kwa ajili ya  kuwa na kumbukumbu ya 
kudumu. “Hali si nzuri ndugu zetu wameungua sana wapo wengine mnaweza 
msiwatambue lakini mnaweza kutambua kwa alama. Wapo wengine walivaa 
bangili, heleni, mkanda havijaungua”.
Kadhalika,
 Waziri Mkuu amesema kama hawajawatambua Serikali imeweka utaratibu wa 
vipomo vya vinasaba, ambapo  kumbukumbu hizo zimechukuliwa na wataalamu 
wetu wa afya. “Kama ukipita ukishindwa kumuona bado tunakuruhusu 
kukupima vinasaba na kulinganisha na vyakwako. Bado haki ya kumpata 
ndugu yako iko pale pale madaktari wapo, mitambo ipo tutachukua vinasaba
 na kuainisha tutatoa nafasi leo hadi saa 10 kufanya utambuzi”.
Amesema
 Serikali inaratibu vizuri jambo hilo lakini kuanzia saa 10 itaruhusu 
wale waliotambuliwa kuchukua mwili lakini kama hawajajipanga vizuri 
itauzika na kama kuna jina litaliandika na kama hakuna jina wataandika 
namba ya vinasaba ili kutoa fursa kwa ndugu siku nyingine waende 
wakapimwe na kuoneshwa kaburi la ndugu yao.
EmoticonEmoticon
Note: Only a member of this blog may post a comment.