Thursday, August 22, 2019

MATUKIO KATIKA PICHA VIJANA MKOANI GEITA WAPATIWA ELIMU YA UJASIRIAMALI

Mchumi Mkuu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Silas Daudi akitoa mada kuhusu Mpango wa Biashara kwa vijana wanajihusisha na shughuli mbalimbali za biashara na ujasiriamali katika Mkoa wa Geita ikiwa ni awamu ya tatu ya Mafunzo ya Ujasiriamali na Usimamizi wa Biashara kwa Vijana wenye umri kati ya miaka 18 hadi 35 yanayosimamiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu.

Baadhi ya Wajasiriamali wakifuatilia kwa makini mada iliyokuwa ikiwasilishwa na mmoja ya watoa mada wakati wa mafunzo ya ujasiriamali na usimamizi wa biashara kwa vijana wenye umri wa miaka 18 hadi 35 yanayoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC).
Mwezeshaji kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Julius Tweneshe akielezea mada kuhusu taratibu za kufungua kampuni wakati wa mafunzo hayo.
Sehemu ya wajasirimali kutoka Mkoa wa Geita wakifuatilia mada iliyokuwa ikiwasilishwa wakati wa mafunzo hayo yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano uliopo katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita.
Afisa Uwezeshaji kutoka Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) Bw. Halidi Mbwana akitoa mada kuhusu masuala ya utafutaji wa vyanzo vya mapato kwa vijana walioshiriki mafunzo hayo Mkoani Geita.
Baadhi ya Wajasiriamali walioshiriki kwenye mafunzo hayo wakijadiliana kazi kwenye vikundi.
Sehemu ya Sekretarieti wakifuatilia mada zilizokuwa zikiwasilishwa na wawezeshaji wakati wa mafunzo hayo yaliyofanyika Mkoani Geita Agosti 22, 2019.



EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.