Thursday, July 27, 2017

MWONGOZO WA URATIBU WA MPANGO KAZI WA TAIFA WA KUTOKOMEZA UKATILI DHIDI YA WANAWAKE NA WATOTO WAJADILIWA.

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Dkt. Hamisi Mwinyimvua  akizungumza na wajumbe wa Kikao cha Makatibu Wakuu cha Kupitia Mwongozo wa Uratibu wa Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto (MTAKUWWA) kilichofanyika tarehe 27 Julai, 2017 katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi hiyo mjini Dodoma.

Baadhi ya Wajumbe wa Kikao cha Makatibu Wakuu cha Kupitia Mwongozo wa Uratibu wa Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto (MTAKUWWA) wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Dkt. Hamisi Mwinyimvua (hayupo pichani) alipokuwa akielezea lengo la Mwongozo huo Julai 27, 2017 Mjini Dodoma.

Baadhi ya Wajumbe wa Kikao cha Makatibu Wakuu cha Kupitia Mwongozo wa Uratibu wa Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto (MTAKUWWA) wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Dkt. Hamisi Mwinyimvua (hayupo pichani) alipokuwa akielezea lengo la Mwongozo huo Julai 27, 2017 Mjini Dodoma.

Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii) Bi. Sihaba Nkinga akionesha kitabu cha Mwongozo wa Uratibu wa Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto (MTAKUWWA) kwa wajumbe wa mkutano wa kupitia na kujadili mwongozo huo kilichofanyika Julai 27, 2017 katika Ukumbi wa Mikutano Ofisi ya Waziri Mkuu Dodoma.

Mkurugenzi wa Sera na Mipango Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bw.Atupele Mwambene akiwasilisha Mwongozo wa Uratibu wa Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto kwa wajumbe wa kikao cha kuujadili na kuupitisha mwongozo huo kilichofanyika tarehe 27 Julai, 2017 katika Ukumbi wa Mikutano Ofisi ya Waziri Mkuu Dodoma.

atibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo akipitia Mwongozo wa Uratibu wa Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto wakati wa kikao cha kuujadili kilichofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Waziri Mkuu Dodoma Julai 27, 2017.

Mkurugenzi wa Uratibu wa Shughuli za Serikali Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Obey Assery (wa kwanza kushoto) akifuatilia uwasilishwaji wa Mwongozo wa Uratibu wa Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto wakati wa kikao cha kuupitia na kuujadili mwongozo huo kilichofanyika Julai 27, 2017 Ofisi ya Waziri Mkuu Dodoma.

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Dkt. Zainabu Chaula akichangia hoja wakati wa kujadili Mwongozo wa Uratibu wa Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto katika kikao cha Makatibu wakuu walipokutana kuujadili na kuupitisha mwongozo huo uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Waziri Mkuu Dodoma.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Amon Mpanju akichangia hoja wakati wa kujadili Mwongozo wa Uratibu wa Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto wakati wa kikao cha kuujadili mwongozo huo kilichjofanyika Julai 27, 2017 Dodoma.

Mkurugenzi wa Anuai za Jamii Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bi. Anne Mazalla akiuliza swali kwa Mwenyekiti wa Kikao cha kujadili Mwongozo wa Uratibu wa Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto (hayupo pichani) Julai 27, 2017 katika Ukumbi wa Mikutano Ofisi ya Waziri Mkuu Dodoma.


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.