Tuesday, July 4, 2017

MHE. WAZIRI MKUU NA MSHINDI WA TUZO YA UINGEREZA

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na Samuel Mwanyika (wa pili kushoto), mshindi wa tuzo ya Stephen Thomas iliyotolewa na Taasisi ya Kimataifa ya Watu wenye Mtindio wa Ubongo (Down's Syndrome Association) ya Uingereza kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma Julai 4, 2017. Wa kwanza kushoto ni Elias Mwanyika (kaka yake Samuel) akiwa na picha iliyoshinda tuzo hiyo na wa kwanza kulia ni Sophie Mshangama ambaye ni mama yake Samuel.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangalla (wa pili kulia) akiwa na Samuel Mwanyika (wa pili kushoto), mshindi wa tuzo ya Stephen Thomas iliyotolewa na Taasisi ya Kimataifa ya Watu wenye Mtindio wa Ubongo ya Uingereza kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma Julai 4, 2017. Wa kwanza kushoto ni Elias Mwanyika (kaka yake Samuel) akiwa na picha iliyoshinda tuzo hiyo na wa kwanza kulia ni Sophie Mshangama ambaye ni mama yake Samuel.

Samuel Mwanyika (19) akiwa ameshika tuzo wakati anatambulishwa kwa Wabunge mjini Dodoma. Samuel alishinda tuzo ya Stephen Thomas iliyotolewa na Taasisi ya Kimataifa ya Watu wenye Mtindio wa Ubongo ya Uingereza bada ya kutuma picha ya pundamilia wawili wakiota jua kwenye hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro. Watoto kutoka nchi 18 walishiriki shindano la picha kwa mwaka 2017.

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Samuel Mwanyika, mshindi wa tuzo ya Stephen Thomas iliyotolewa na Taasisi ya Kimataifa ya Watu wenye Mtindio wa Ubongo (Down's Syndrome Association) ya Uingereza kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma Julai 4, 2017. Katikati ni Mama wa mtoto huyo Sophie Mshangama


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.