Tuesday, November 14, 2017

SERIKALI YAWAJENGEA UWEZO WAJUMBE WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE MASUALA YA UKIMWI

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira, Kazi, Vijana na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akitoa ufafanuzi wa masuala ya Ukimwi kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge inayoshughulikia masuala ya UKIMWI wakati wa warsha ya wajumbe wa kamati hiyo iliyofanyika Bungeni Dodoma Novemba 14, 2017.

Mkurugenzi wa Utafiti na Tathimini Tume ya Taifa ya kudhibiti Ukimwi (TACAIDS) Dkt. Jerome Kamwela akiwasilisha mada ya hali ya UKIMWI nchini kwa Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge inayoshughulikia masuala ya Ukimwi wakati wa warsha kwa wajumbe wa kamati hiyo iliyofanyika tarehe 14 Novemba, 2017.
Mkurugenzi Mtendaji Tume ya Taifa ya kudhibiti Ukimwi Dr. Leonard Maboko akichangia hoja kuhusu masuala ya Ukimwi wakati wa Warsha ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Masuala ya UKIMWI iliyofanyika Mjini Dodoma.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI Mhe. Daniel Mtuka akifafanua jambo wakati wa warsha kwa wajumbe wa kamati hiyo kuhusu masuala ya Ukimwi nchini iliyofanyika Bungeni Dodoma Novemba 14, 2017.
Mmoja wa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI Mhe. Martha Mlata akichangia hoja wakati wa warsha iliyoandaliwa na Tume ya Taifa ya kudhibiti Ukimwi kuhusu masuala ya Ukimwi iliyofanyika Mjini Dodoma. 
Mmoja wa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI Mhe.Zainab Bullu akifafanua jambo wakati wa warsha kwa wajumbe wa kamati hiyo iliyoandaliwa na Tume ya Taifa ya kudhibiti Ukimwi.

Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI Mhe. Masoud Abdalla salim akichangia hoja wakati wa warsha ya Wajumbe wa kamati hiyo mjini Dodoma.


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.