Friday, November 10, 2017

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AKUTANA NA KATIBU MKUU KIONGOZI MJINI DODOMA

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Injinia John Kijazi wakati alipomtembelea Waziri mkuu ofisini kwake mjini Dodoma leo Novemba 10/2017 kwa mazungumzo ya kikazi.Katikati ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu  Sera Bunge,Kazi Ajira,Vijana na Walemavu Jenista Mhagama

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akimfafanulia jambo Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Mara Joyce Sokombi.(chadema) wakati wa Majadiliano ya Mapendekezo ya Mpango  wa Taifa wa Fedha kwa Mwaka 2018/2019 bungeni Dodoma leo Novemba 10/2017.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akimsikiliza Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Singida Martha Mlata (CCM) wakati wa Majadiliano ya Mapendekezo ya Mpango  wa Taifa wa Fedha kwa Mwaka 2018/2019 bungeni Dodoma leo Novemba 10/2017.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akimsalimia Mtoto Ivan (miezi7)akiwa katika Viwanja vya Bunge na Mama yake Mariam Zablon kutoka Bukombe mkoani Geita walipotembelea bungeni Dodoma leo Novemba 10/2017 kujionea shughuli za Bunge.


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.