Wednesday, February 13, 2019

NAIBU WAZIRI IKUPA ATEMBELEA KUKUNDI CHA WAJASIRIAMALI WENYE ULEMAVU NA SHULE YA VIZIWI DODOMA


Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia (Watu wenye Ulemavu) Mhe. Stella Ikupa akitengeneza viatu vya wazi (Makobazi) alipotembelea Chama cha Walemavu Salungai kilichopo Kata ya Ipagala, Jijini Dodoma. (Kulia) ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Dodoma Mjini Bw. Edward Mpogolo.
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia (Watu wenye Ulemavu) Mhe. Stella Ikupa akinunua viatu vya wazi aina ya Makobazi kwa Chama cha Walemavu Sulungai (CHAWASU) alipotembeleaa Kikundi hicho kilichopo Kata ya Ipagala kujionea shughuli zinazofanywa na wajasiriamali hao.
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia (Wenye Ulemavu) Mhe. Stella Ikupa  akieleza jambo wanafunzi wa shule viziwi iliyopo Jijini Dodoma(hawapo pichani), alipotembelea shule hiyo kukagua utekelezaji wa masuala ya Watu wenye Ulemavu.
Mwananfunzi mwenye Uziwi wa darasa la Tatu, Shadia Kizamo akitaja jina la Waziri Mkuu wa Jamhuri y Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa kwa lugha ya alama swali aliloulizwa na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia (Watu wenye Ulemavu) Mhe. Stella Ikupa  (hayupo pichani).
Mwananfunzi mwenye Uziwi wa darasa la Saba, Eliabi Chilongola akimweleza kwa lugha ya alama Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa, teknolojia aliyoivumbua ya Umwagiliaji.
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa akimsikiliza Mratibu wa Shule maalumu ya Viziwi Dodoma, Bw. Robin Donilergoed (wa pili kutoka kulia) alipokuwa akikagua miundombinu ya Shule hiyo.
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa akiwa kwenye picha ya pamoja na wanafunzi wenye Uziwi wanaojishughulisha na ufundi wa Ushonaji.


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.