Sunday, December 18, 2016

DKT. POSSI AITAKA JAMII KUHESHIMU HAKI ZA WATU WENYE ULEMAVU.

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Watu wenye Ulemavu) Mhe. Dkt. Abdallah Possi akionesha namna ya kutumia Kurunzi ya mwanga wa jua kwa baadhi ya wazee wenye ukoma wanaoishi katika Kambi ya Mkaseka Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara na kuwapatia wazee hao kurunzi 20 kwa kila nyumba.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Watu wenye Ulemavu) Mhe. Dkt. Abdallah Possi (wa kwanza kushoto) akiwa katika ziara ya kuangalia maeneo ya shule ya Masasi inayohudumia wanafunzi wa mahitaji maalum wakati wa ziara yake mkoani Mtwara.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Watu wenye Ulemavu) Mhe. Dkt. Abdallah Possi akitoa maelekezo kwa Mkuu wa Wilaya ya Masasi Mhe. Selemani Mzee (wa kwanza kulia) wakati wa ziara yake katika shule ya Masasi yenye kuhudumia wenye ulemavu Mkoani Mtwara.




EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.