Saturday, November 3, 2018

MAJALIWA AKAGUA UJENZI WA RELI YA KISASA YA SGR

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la reli Tanzania  (TRC), Masanja Kadogosa kuhusu ujenzi wa Reli ya SGR wakati alipotembelea kambi ya Kampuni ya Yapi Markezi inayojenga Reli hiyo,  katika eneo la Shaurimoyo jijini Dar es salaam, Novemba 3, 3018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akikagua maandalizi ya  ujenzi wa madaraja  ya  kupitisha treni  juu  wakati alipotembelea kambi ya Kampuni ya Yapi Merkezi inayojenga reli ya Kisasa ya SGR   Oktoba 3, 2018. Kambi hiyo ipo eneo la Shaurimoyo jijini Dar es salaam. Wapili kushoto ni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi, Isack Kamwelwe. 

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua kazi ya utengenezaji mataluma ya reli ya SGR wakati alipotembelea Kambi ya Kampuni ya Yapi Merkezi katika eneo la Soga mkoani Pwani, Oktoba 3, 2018. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhandisi Evarest Ndikilo.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua utandikaji wa  reli ya SGR katika eneo la Soga mkoani Pwani, Oktoba 3, 2018.  Wapili kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC), Masanja Kadogosa.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiagana na  wafanyakazi wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) pamoja na wafanyakazi wa Kampuni ya Yapi Merkezi inayojenga reli ya kisasa ya SGR kati ya Dar es slaam na Morogoro baada ya kukagua ujenzi wa reli hiyo katika eneo la Soga mkoani Pwani,  Oktoba 3, 2018.  Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa TRC, Masanja Kadogosa.


EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.