Monday, September 2, 2019

KAMATI ELEKEZI YA TAIFA YA ULINZI WA WANAWAKE NA WATOTO YAKUTANA DODOMA

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Uwekezaji) Bi.Dorothy Mwaluko pamoja na Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. John Jingu wakipitia muhtasari wa kikao kilichopita wakati kikao cha Kamati Elekezi ya Taifa ya Ulinzi wa Wanawake na Watoto kilichofanyika mkoani Morogoro.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Amon Mpanju akichangia hoja kuhusu sheria mbalimbali zinazowalinda watoto dhidi ya ukatili wakati wa kikao hicho.
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Uwekezaji) Bi.Dorothy Mwaluko akizungumza jambo wakati wa ufunguzi wa kikao cha Kamati Elekezi ya Taifa ya Ulinzi wa Wanawake na Watoto kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Magadu JWTZ mkoani Morogoro, kushoto ni Katibu mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. John Jingu.
Sehemu ya wajumbe wa kikao cha Kamati Elekezi ya Taifa ya Ulinzi wa Wanawake na Watoto wakifuatilia hoja za mwenyekiti wa kikao hicho ambaye ni Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Uwekezaji) Bi.Dorothy Mwaluko (hayupo pichani).
Sehemu ya wajumbe wa sekretariati wakifuatilia hoja na michango ya wajumbe wakati wa kikao hicho.
Sehemu ya wajumbe wa kikao cha Kamati Elekezi ya Taifa ya Ulinzi wa Wanawake na Watoto wakifuatilia hoja za mwenyekiti wa kikao hicho ambaye ni Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Uwekezaji) Bi.Dorothy Mwaluko (hayupo pichani).
Sehemu ya wajumbe wa kikao cha Kamati Elekezi ya Taifa ya Ulinzi wa Wanawake na Watoto wakifuatilia hoja za mwenyekiti wa kikao hicho ambaye ni Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Uwekezaji) Bi.Dorothy Mwaluko (hayupo pichani)

Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bw. Atupele Mwambene akiwasilisha taarifa ya Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto wakati wa kikao hicho.
Muwakilishi kutoka Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) Bi. Zainabu akieleza namna wanavyotatua masuala ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto kupitia teknolojia ya mitandao wakati wa kikao hicho.

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Uwekezaji) Bi.Dorothy Mwaluko (wa tatu kutoka kushoto) pamoja na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Dkt. Laurean Ndumbaro (katikati), Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Dkt. John Jingu (wa pili kutoka kushoto), na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Bw.Amon Mpanju (wa tatu kutoka kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Kamati Elekezi ya Taifa ya Ulinzi wa Wanawake na Watoto mara baada ya kumaliza kikao hicho.

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Uwekezaji) Bi.Dorothy Mwaluko akiteta jambo na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Dkt. Laurean Ndumbaro mara baada ya kufunga kikao hicho.




EmoticonEmoticon

Note: Only a member of this blog may post a comment.